'Ni siku ya Mdahalo na Ngoni day'
Leo Februari 25, 2026 ni siku ya Mdahalo na Ngoni Day katika mwendelezo wa matukio kuelekea kilele cha Tamasha la Kumbukizi ya miaka 120 ya Mashujaa wa Vita vya Majimaji Songea.
Katika siku hii kumefanyika Mdahalo eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Shule ya Sekondari Madaba.
Mgeni rasmi alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Ndug. Joseph Mrimi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Songea.
Huko Maposeni kulifanyika tamasha la siku ya Wangoni (Ngoni day) kama kumbukizi ya mashujaa waliopigaga katika vita vya Majimaji likihudhuriwa na wageni kutoka Malawi, Zambia na Africa Kusini.
Mgeni rasmi alikuwa Mhe. Abraham Mbunda Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
I




















0 Comments