Header Ads Widget

NETANYAHU ATISHIA KULIPIZA KISASI HUKU HAMAS IKILAUMU ISRAEL 'KUWALENGA WATOTO KATIKA KIJIJI CHA TUFAH'

 


Afisa wa zima moto amesimama katika eneo lililoshambuliwa kutoka Ukanda wa Gaza kuelekea Israel huko Ashkelon.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameagiza ‘’kulipiza kisasi’’ baada ya shambulizi la maroketi kutoka ukanda wa Gaza Jumapili.

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa Netanyahu alizungumza na Waziri wa Ulinzi Israel Katz kutoka kwenye ndege hiyo kuelekea Washington.

Jeshi la Israel limesema liligundua roketi 10 zilizorushwa kutoka Ukanda wa Gaza kuelekea kusini mwa Israel, ambazo nyingi zilinaswa, huku ving'ora vya mashambulizi ya anga vikisikika huko Ashkelon na Ashdodi.

Tishio la Netanyahu linajiri baada ya wanamgambo wa Hamas kutangaza kuwaa wamerusha makombora kutoka Gaza kuelekea Israel.

Mtu mmoja amejeruhiwa katika mji wa Ashkelon.

Jeshi la Israel nalo limesema limemuua mpalestina mmoja na kuwajeruhi wawili katika mji wa Turmus Ayya katika ukingo wa magharibi.

Hayo yanajiri huku kukiwa na juhudi za kufufua mazungumzo ya kusitisha mapigano Gaza.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI