Header Ads Widget

KWANINI KANDE, MBEGE NA MACHALARI NI BORA KULIKO PIZZA NA BURGER?

 



Utafiti mpya uliofanyika nchini Tanzania na kuchapishwa na jarida kubwa la Nature Medicine la nchini Uingereza mwishoni mwa wiki, umebaini kuwa lishe ya asili ya Kiafrika ina faida kubwa kiafya kuliko lishe ya Kimagharibi.

Utafiti huo ulioanza kufanyika mwaka 2021 umefanywa na watafiti wa Chuo Kikuu cha KCMC na Taasisi ya Utafiti ya KCRI na kubaini kwamba mabadiliko ya lishe ya wiki mbili yananatosha kuleta mabadiliko ama chanya ama hasi katika mfumo mzima wa kinga ya mwili.

Utafiti huo ulioshirikisha watu 77 wenye afya njema kutoka maeneo ya mijini na vijijini, ulilenga kuangalia athari za vyakula vya asili dhidi ya vyakula vya kisasa na vya mjini vinavyofanana na vya Magharibi kwa afya ya mwili. Ukizingatia mfumo wa kinga ya mwili na jinsi unavyoweza kukabiliana na magonjwa.

"Tulifanya utafiti huu kwa kushirikiana na Taasisi mbalimbali za kimataifa, lakini tukalenga Moshi, Kilimanjaro kwa sababu watu bado wanatumia vyakula vya jadi," anasema Godfrey Temba, mtafiti kutoka timu ya utafiti ya KCMC, ambaye pia Daktari wa kinga ya mwili.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI