Header Ads Widget

KUONDOLEWA KWA MISAADA YA USAID KWAWAWEKA WANAWAKE WAJAWAZITO HATARINI- UN



 Umoja wa Mataifa umeonya kuwa kupunguzwa kwa bajeti za misaada kutahujumu hatua zilizokuwa zimefanikishwa za kupunguza vifo vya kina mama wakati wa kujifungua.

Ripoti iliyotolewa na shirika la afya duniani WHO inasema vifo vitokanavyo na uja uzito na kujifungua vilikuwa vimeshuka kwa asilimia arobaini katika karne hii lakini wataalam wanahofu kuwa huenda vifo hivyo vikaongezeka tena kutokana na kusitishwa kwa misaada ya kigeni.

Wanawake walio na uja uzito hukumbwa na changamoto nyingi hasa katika mataifa yanayokumbwa na mizozo kama Chad, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Nigeria na Somalia.

Mnamo mwaka 2020,WHO ilirekodi vifo elfu mia mbili sitini ikiwa ni sawa na mwanamke mmoja kufariki dunia kila baada ya dakika mbili kutokana na changamoto wakati wa kujifungua.

Kifo cha uzazi ni kile kinachosababishwa na matatizo wakati wa ujauzito au ndani ya wiki sita baada ya mwisho wake.

Sababu zinazoongoza ni pamoja na kutokwa na damu nyingi, maambukizi kama vile malaria, matatizo wakati wa kujifungua, na utoaji mimba usio salama.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI