Header Ads Widget

MICHELLE OBAMA APUUZA UVUMI KUHUSU TALAKA KWENYE NDOA YAKE

 

Michelle Obama, mke wa rais wa zamani wa Marekani Barack Obama amezungumzia uvumi kuwa ndoa yake inaelekea kuvunjika.

Michelle hajaandamana na mumewe kwenye hafla kadhaa za kitaifa- ikiwa ni pamoja na kuapishwa kwa Donald Trump na mazishi ya Rais wa zamani Marekani Jimmy Carter - na kuchochea uvumi kwamba wanaweza kutengana.

Bila kutaja matukio haya kwa uwazi, Bi Obama aliambia podcast ya Work in Progress iliyoandaliwa na muigizaji Sophia Bush kwamba sasa yuko katika nafasi ya kudhibiti shajara yake mwenyewe kama "mwanamke mzima".

Alisema kuwa watu hawaamini kwamba "anajifanyia uamuzi" wake mwenyewe na badala yake "ilibidi waibue hoja kuwa mimi na mume wangu tunatalikiana".

Bi Obama alikiri kuwa alijihisi kama mkosa kwa kujiondoa katika majukumu fulani.

"Hilo ndilo jambo ambalo sisi kama wanawake, nadhani tunapambana nalo," alisema.

"Hili ni wazi, kiasi kwamba mwaka huu watu hawakuweza hata kufahamu kuwa nilikuwa na uamuzi binafsi, ikabidi wafikirie kuwa mimi na mume wangu tunatalikiana.

"Huyu hawezi kuwa mwanamke anayejifanyia maamuzi yake mwenyewe, sivyo? Lakini ndivyo jamii inavyotufanyia."

Bi Obama pia alisema katika podcast hiyo: "Niliamua kufanya kile ambacho kilikuwa bora kwangu. Sio kile nilichopaswa kufanya. Sio kile watu wengine walitaka nifanye."

Japo kutokuwepo kwake kwenye hafla ya kuapishwa kwa Rais Trump kulionekana kama kinyume na desturi, alitoa hotuba ya hali ya juu katika Kongamano la Kitaifa la chama cha Democratic (DNC) mwaka jana.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI