Header Ads Widget

MABADILISHANO YA WAFUNGWA YA MAREKANI NA URUSI: ALIYEFUNGWA JELA KWA KUSAIDIA UKRAINE AACHILIWA

 


Raia wa Urusi mwenye asili ya Marekani ameachiliwa huru katika mabadilishano ya wafungwa kati ya Moscow na Washington.

Ballerina Ksenia Karelina, mkazi wa Los Angeles, alikuwa gerezani nchini Urusi kwa zaidi ya mwaka mmoja, baada ya kukamatwa katika jiji la Yekaterinburg mapema 2024.

Alipatikana na hatia ya uhaini kwa kutoa pesa kwa shirika la misaada lenye makao yake makuu nchini Marekani linalotoa msaada wa kibinadamu kwa Ukraine na alihukumiwa kifungo cha miaka 12.

Kwa kubadilishana, Marekani iliripotiwa kumwachilia Arthur Petrov, raia mwenye uraia mara mbili wa Ujerumani-Urusi aliyekamatwa Cyprus mwaka wa 2023. Alishtakiwa kwa kusafirisha vifaa vidogo vya kielektroniki kwenda Urusi kwa watengenezaji wanaofanya kazi na jeshi la Urusi kinyume cha sheria.

Mabadilishano ya wafungwa yalifanyika Abu Dhabi asubuhi ya Alhamisi.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio alithibitisha kuwa Bi Karelina alikuwa "kwenye ndege akirejea nyumbani Marekani."

Aliongeza kuwa "amezuiliwa kimakosa na Urusi kwa zaidi ya mwaka mmoja".

Ni mara ya pili kubadilishana wafungwa kati ya Urusi na Marekani katika muda wa chini ya miezi miwili.

Mnamo Februari, raia wa Urusi Alexander Vinnik - ambaye alifungwa katika jela ya Marekani kwa mashtaka ya utakatishaji fedha - aliachiliwa kwa kubadilishana na kuachiliwa kwa mwalimu wa shule wa Marekani Marc Fogel.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI