Header Ads Widget

KOREA KUSINI KUFANYA UCHAGUZI WA RAIS JUNI 3

 



Korea Kusini itafanya uchaguzi wa rais tarehe 3 Juni, kaimu kiongozi wake amesema, baada ya mahakama ya kikatiba ya nchi hiyo kuunga mkono hoja ya kumwondoa aliyekuwa Rais Yoon Suk Yeol.

Bunge la nchi hiyo lilipitisha hoja ya kumuondoa madarakani Rais Yoon mnamo mwezi Desemba kwa kutangaza sheria ya kijeshi iliyoshtua nchi.

Mahakama iliidhinisha kushtakiwa kwake tarehe 4 Aprili, na hivyo kufungua njia ya kufanyika kwa uchaguzi wa haraka ndani ya siku 60.

Kaimu rais Han Duck-soo alitangaza tarehe ya uchaguzi Jumanne, akisema nchi inahitaji "kupona haraka" na kusonga "mbele".

Tangazo la Yoon la sheria ya kijeshi liliitumbukiza Korea Kusini katika hali ya sintofahamu ya kisiasa na kusababisha mgawanyiko mkubwa nchini humo.

"Ninaomba radhi kwa kuleta mkanganyiko na wasiwasi kwa wananchi katika kipindi cha miezi minne iliyopita, na kwa kukabiliwa na hali hii ya kusikitisha katika nafasi ya urais," Han alisema.

Yoon alirejelea vitisho kutoka kwa "vikosi vinavyopinga serikali" na Korea Kaskazini alipotangaza sheria ya kijeshi. Lakini baada ya muda mfupi kupita, ilibainika wazi kuwa hatua hiyo haikuchochewa na vitisho vya nje bali matatizo yake ya kisiasa ya ndani.

Ameshtakiwa kwa kosa tofauti la uasi mbele ya mahakama ya jinai.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI