Header Ads Widget

FAMILIA ZAANZA KUWAAGA WALIOFARIKI KATIKA MKASA WA UKUMBI WA BURUDANI DOMINICAN

 


Maelfu ya watu wamejitokeza katika Jamhuri ya Dominica kutoa heshima zao za mwisho kwa mwanamuziki mashuhuri Rubby Perez aliyefariki dunia katika mkasa wa paa la ukumbi wa burudani lililomuangukia pamoja na mashabiki wake siku ya Jumanne wiki hii.

Takriban watu mia mbili ishirini walikufa katika mkasa huo na serikali imetangaza kuundwa kwa jopo la wachunguzi kuchunguza mkasa huo uliokumba klabu ya Jet Set.

Binti ya mwanamuziki huyo Zulinka Peres aliyekuwa pia akitumbuza na babake wakati wa mkasa amewaeleza waombolezaji kuwa ana bahati yuko hai.

"Mimi na mume wangu ni mashahidi wa muujiza kwasababu tulikuwa kando yake.Sisi nimanusura wa mkasa huo.Nilikiona kilichojiri pale,hakuna atakayenisimulia.Namshukuru Mungu na mume wangu niko hai kwasababu alinifunika na mwili wake na ndiyo maana niko hapa, asema Zulinka Peres.

Mamlaka haijabaini sababu ya kuporomoka kwa paa la klabu ya burudani, ambapo sherehe yake ya kitamaduni ya "Merengue Monday" ilikuwa ikifanyika.

"Ilikuwa ghafla," alisema meneja wa Rubby Pérez, Enrique Paulino, ambaye alinusurika. "Nilifikiri lilikuwa tetemeko la ardhi, kwa hiyo nilijitupa chini na kufunika kichwa changu... Mmoja wa wapiga saksafoni wetu alikufa. Tulijaribu kufika eneo ambalo Rubby alikuwa, lakini vifusi vilikuwa vimetapakaa kila mahali."

Haya yakijiri serikali ya Dominica imetangaza kuwa shughuli za uokozi zimekamilika na taifa linaendelea kuomboleza na kufarijiana.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI