Msafara wa My Tanzania Roadshow 2025 umeanza kwa kishindo, kwa siku ya kwanza katika jiji la Cologne nchini Ujerumani . Likiunganisha mawakala wa utalii wa Tanzania na mawakala wa kimataifa katika miji mikubwa ya Ulaya Magharibi. Lengo ni Kutangaza vivutio vyetu vya kipekee na kuvutia wageni zaidi!
Kwa ushirikiano wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), TANAPA, NCAA, na sekta binafsi, tunahakikisha kuwa Tanzania inasalia kuwa chaguo namba moja kwa watalii duniani.
Ulaya ni soko muhimu kwa utalii wetu, na kupitia jitihada hizi, tunazidi kupanua wigo wa watalii wanaokuja kutembelea vivutio mbalimbali nchini m ikiwemo hifadhi za Taifa.
Tanzania Unforgettable
0 Comments