Header Ads Widget

WENYEVITI WA MITAA, WAJUMBE WA MANISPAA YA LINDI WALA KIAPO BAADA YA UCHAGUZI

Na Hadija Omary 

Lindi....Jumla ya wenyeviti na wajumbe wa Serikali za mitaa na vitongoji 1953 wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani Lindi  wamekula kiapo cha uaminifu na uadilifu Katika majukumu Yao mapya 

Zoezi Hilo limeongozwa  na Hakimu Mkazi Mahaka ya Mwanzo  Illuminata Lutakana mara baada ya viongozi hao kushinda uchaguzi uliofanyika Novemva 27 mwaka huu.


Akizungumza baada ya zoezi  hilo liliofanyika katika Ukumbi wa Donkey Hall   Mkuu wa Wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva amewataka Wenyeviti wa Mitaa,Vijiji , na Wajumbe wajumbe wa Serikali za mitaa na Vijij kufanya kazi kwa uadilifu na uzalendo katika kuwatumikia wananchi ili kuleta maendeleo katika maeneo yao.

Mwanziva amesema viongozi hao ndio wanakutana na wananchi na kugundua changamoto zao hivyo wanapaswa kushughulika na mambo ya wananchi waliokuchagua bila kujali itikadi za vyama na dini zao.


Naye Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Juma Mnwele amewapongeza viongozi hao kuaminiwa na kuchaguliwa na kuwataka kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, hasa kuepuka kuingilia majukumu ya kisheria ya vyombo vingine ikiwemo uuzaji wa viwanja.


Mwishoo

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI