Header Ads Widget

MATOKEO YA UCHAGUZI NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YA MUSOMA VIJIJINI

 


Jimbo la Musoma Vijijini:

Jumla: Kata 21  Vijiji 68  Vitongoji 374

Matokeo:

(i) Vijiji 66: CCM    

     Vijiji 2: CHADEMA

Ushindi wa CCM: 97.06%


(ii) Vitongoji 357: CCM  

      Vitongoji 17: CHADEMA 

Ushindi wa CCM: 95.45%


*Maendeleo ya wote:*

Matokeo ni hayo. Tusisahau kwamba sisi Musoma Vijijini huwa hatuna ubaguzi wa kisiasa na hatuna ubaguzi wa aina yo yote ile!


*Utekelezaji wa miradi ya maendeleo:*


Muhimu kwetu ni maendeleo shirikishi kwa manufaa ya jamii yote ndani ya vitongoji, vijiji na kata zetu zote.


Kuanzia wiki ijayo tunaendelea na utekelezaji wa miradi yetu iliyobuniwa na kuanza kutekelezwa kwa kutumia nguvu za wanavijiji. Baadhi ya miradi hiyo imeanza kupata michango ya fedha kutoka Serikalini


Miradi ni mingi, baadhi yake ni hii ifuatayo:


(i) ujenzi wa maabara 3 za masomo ya sayansi kwa kila sekondari ya Kata


(ii) ujenzi wa sekondari mpya kumi (10)


(iii) ujenzi wa shule shikizi nane (8) mpya


(iv) ujenzi wa zahanati mpya kumi na saba (17)

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI