Header Ads Widget

DK.MPANGO APIGA KURA ATAKA VIONGOZI WANAOCHAGULIWA WASIMAMIE MAENDELEO

 

Na Fadhili Abdallah,Kigoma 

MAKAMU WA Raisi Dk.Philip Mpango amepiga kura nyumbani kwake katika kijiji cha Kasumo wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma kwa ajili ya kuchagua viongozi wa serikali za mitaa huku akitaka wananchi kuchagua kwa kuzingatia viongozi wenye maono ya kuwaletea maendeleo.

Aidha Dk.Mpango Amesema kuwa  ni muhimu kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa viongozi hao kwa

kujitokeza kuwaunga mkono katika shughuli za maendeleo watakazosimamia.

Amesema viongozi wa serikali za

mitaa ni viongozi wa ngazi ya msingi wanaobeba dhamana ya kuwaongoza wananchi

kupata maendeleo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na baadaye

Sambamba na hilo Makamu wa Rais ametoa wito kwa viongozi watakaochaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa


kutumia vema nafasi hizo kuwaletea wananchi maendeleo.

Makamu wa Rais amewapongeza wanakijiji wote wa kijiji cha Kasumo waliojitokeza katika kupiga kura kwenye  uchaguzi huo muhimu.

kwa kuwa ni muhimu kwa msingi wa maendeleo

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI