Header Ads Widget

SHANGWE NA VIGELEGELE VYA TAWALA KAGERA BAADA YA KUIBUKA MSHINDI WA MBIO ZA MWENGE 2024

 

Na Shemsa Mussa 
Kagera .

Wananchi Mkoani Kagera pamoja na Viongozi mbali mbali wamesikika wakipiga Vigelegele na shangwe nyingi wakati wakimpokea Mkuu wa Mkoa wa huo Hajat Fatma Mwassa katika Uwanja wa ndege Bukoba akitokea Mkoani Mwanza akiwa amebeba kikombe na cheti maalum baada ya Mkoa wa Kagera kuibuka kinara Katika mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2024.

Baada ya kiongozi huyo kuwasili Katika viwanja hivyo alisikika akisema Kagera piga kelele itoshe kusema Kagera Baba lao huku shangwe zikisikika kila kona Mkoani humo.


Rc Mwassa alipopata nafasi ya kuzungumza na umati uliofika eneo hilo alisema" nawapongeza Wananchi wote kwa ushindi wa Mwenge naamini ushindi huu hauwezi kupatikana kwa mtu mmoja mmoja bali ni kwa ushirikiano wa wote hongereni.


Aidha aliongeza kuwa juhudi za ushindi huo zilitokana na wanaKagera kujitoa kwa nguvu zao zote maarifa yao yote na akili zao huku wakiikataa nafasi ya nyuma na kuitaka nafasi ya mbele ambapo wameipigania na kuipata.

Mkoa wa Kagera uliibuka kinara kwa kupata  nafasi ya kwanza kwa kufanya vizuri katika kusimamia shughuli za maendeleo na shughuli za mbio za Mwenge wa uhuru.

Ushindi huo ulitangazwa kupitia  kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2024 Mkoani Mwanza kilichoendana na hitimisho la wiki ya Vijana na kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere oktoba  14, 2024.

Aidha ujumbe Mkuu wa mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2024 ulijikita kwenye uhifadhi wa Mazingira na uhamasishaji wa uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Hata hivyo Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 zitazinduliwa rasmi Mkoani Pwani na kuzimwa Mkoani Mbeya ambapo ndio Mkoa  utakaofanya shughuli za kilele cha mbio za Mwenge.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI