Header Ads Widget

JKT LAWATAHADHARISHA WANANCHI KUHUSU MATAPELI NAFASI ZA JKT

 



Na Hamida Ramadhan, Matukio Daima App Dodoma


JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limewaita vijana wote wa Tanzania Bara na Visiwani kujiunga na nafasi za mafunzo ya jeshi hilo kwa kujitolea huku likiwataadharisha wananchi kuepuka matapeli kwani mafasi hizo ni bure Haziuzi


Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dodoma Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala (JKT) Kanali Juma Mrai amesema utaratibu wa Vijana kujiunga na hatimaye kuchaguliwa na mafunzo hayo unaratibiwa na ofisi za wakuu wa Mikoa na Wilaya ambapo mwombaji anaishi. 


" Usaili wa Vijana kujiunga na mafunzo ya jeshi la kujeunga Taifa kwa kujitolea utaanza  tarehe 01Oktoba 2024 kwa Mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani, " Amesema. 


Na Kuongeza "Vijana watakaoteuliwa watatakiwa kuripoti kwenye makambi ya jeshi la kujenga Taifa kuanzia tarehe 1 Novemba 2024 hadi Novemba 3 ,2024," Amesema Kanali Juma Mrai. 



Aidha amesema Jeshi la kujenga Taifa linapenda kuwataarifu Vijana watakaopata fursa hiyo kuwa jeshi la kujenga Taifa kuwa halitoi ajira, pia halihusiki kuwatafutia ajira katika Asasi, vyombo vya ulinzi na Usalama na mashirika mbalimbali ya Serikali  na ya sio ya kiserikali. 


" Hivyo ifahamike kwamba Jeshi hutoa mafunzo ambayo yatawasaidia  Vijana kujiajiri  wenyewe Mara baada ya kumaliza mkataba wao na jeshi la kujenga Taifa (JKT) , "Amesema Kanali Mrai. 


Hata hivyo Kanali Mrai  amesema Jeshi hilo halitahusika na utapeli wowote ambao utatokea na badala yake wafuate taratibu husika katika Ofisi ambazo zimeainishwa. 


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI