Header Ads Widget

MBUNGE KASAKA AIBANA SERIKALI KUPUNGUZA BEI YA UMEME

  


Mbunge wa Jimbo la Lupa ,Wilaya ya Chunya  Mkoa wa Mbeya Masache Njelu  Kasaka  ameibana  Serikali iangalie namna ya kukokotoa upya bei ya umeme baada ya mradi wa kufua nishati hiyo wa Julius Nyerere (JNHPP)kukamilika ili kupunguza gharama kwa wananchi.


Kasaka akiuliza swali bungeni amehoji "Serikali  haioni haja ya kupitia upya ukokotoaji wa bei za unit na baadaye kushusha bei ili kuleta nafuu kwa mtanzania "


Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga amesema, gharama za umeme si za uzalishaji pekee bali zinahusisha usambazaji na usafirishaji na uwekezaji.


Pia Kasaka ameisihi serikali kufanya jitihada za haraka kusambaza umeme maeneo ya uchimbaji wa dhahabu (migodini ) Ili kurahisisha uzalishaji kwa njia za kisasa.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI