Header Ads Widget

RAIS DKT. SAMIA AGUSWA NA MWANAFUNZI MLEMAVU, AAGIZA KUPATIWA MGUU BANDIA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan aguswa 
na Mwanafunzi wa Darasa la Tatu Shule ya Msingi Tunduma, Ebenezer Mwakasyele (8) ambaye ni mlemavu na kuagiza Ofisi yake pamoja na Wizara ya Afya kuhakikisha Mtoto huyo anatengenezewa mguu wa bandia mara moja.

Mwanafunzi huyo alikuwa ni miongoni mwa watu waliojitokeza kumlaki na  kumsikiliza Rais wakati akiwahutubia wananchi wa  Tunduma, Mkoani Songwe, leo Julai 18, 2024.

Rais Dkt. Samia alisimama katika mji huo wa Tunduma kwa lengo la kuwasalimia   wananchi  akiwa njiani kuelekea Dodoma Mara baada ya Kumaliza Ziara yake ya kikazi katika  mikoa ya Katavi na  Rukwa.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI