Header Ads Widget

BREAKING :MAHAKAMA YA RUFAA YAMREJESHA WAKILI MWAMBUKUSI KUGOMBEA URAIS TLS,MWENYEWE ATOA NENO

WAKILI maarufu wa  kujitegemea nchini Boniface Mwabukusi amesema wakati anapata taarifa ya kuenguliwa kugombea nafasi ya Rais wa TLS (Chama cha Mawakili Tanganyika) na kamati ya rufani ya chama hicho hakuamini kama Mawakili wenzake wanaweza kufanya dhulma ya aina hiyo dhidi yake kwa kuwa aliona wazi maamuzi hayo hayakuwa ya haki na hayakufuata misingi ya kisheria ndio maana hata wahusika hawakumpatia nafasi ya kujitetea


Wakili Mwabukusi amezungumza hayo leo, Ijumaa Julai 26.2024 mbele ya wanahabari muda mfupi baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam kutengua maamuzi ya kamati hiyo na kumrejesha Wakili Mwabukusi kugombea nafasi ya Rais wa TLS katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao


Kwa upande wake Wakili Jebra Kambole aliyekuwa anamtetea Wakili Mwabukusi katika kesi hiyo sambamba na Mawakili wenzake 18 ametoa wito kwa mamlaka mbalimbali zinazotoa maamuzi nchini ni lazima zizingatie misingi ya kisheria katika maamuzi yao badala ya kutumia nafasi walizonazo kuumiza wengine,

Chanzo:Jambo

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI