Header Ads Widget

WANAHARAKATI WAPAZA SAUTI KUKAMATWA KWA MWANDISHI DINNA MANINGO NA WENFINE


 TAARIFA KUHUSU MWENENDO WA UHURU WAKUJIELEZA NCHINI KUFUATIA 

KUKAMATWA KWA MWANDISHI WA HABARI DINNA MANINGO NA 

WANAHARAKATI WENGINE WA KUPIGANIA UHURU WA KUJIELEZA

Ndugu Wananchi na Wapenda Haki ,tunawasalimu !

Ndugu Wananchi,,Hivi karibUuni kumeibuka vitendo vya ukamataji wa wanaharakati mbalimbali 

wanaotumia Uhuru na Haki yao ya Kikatiba kutoa taarifa na maoni mbalimbali.Miongoni mwa 

wanaharakati ambao hivi karibuni wamekumbana na kadhia hizo ni pamoja na Malisa Godlisten 

ambaye mpaka tunaaadaika tamko hili ana kesi Mahakama ya Kisutu Jijijini Dar es Salaam na pia 

anakabiliwa na mashitaka matatu mkoani Kilimanajaro yote yakihusiana na Uhuru wa Kujieleza kwa 

kutumia mitandao ya kijamii.Mwanaharakati mwingine ni Boniface Jacob ambaye naye anakabiliwa 

na mashitaka mawili kwenye Mahakama ya Kisutu Jijini Dares Salaam na wengine ambao 

wamekumbwa na ukamataji huu ni pamoja na Mwandishi wa Hbari Dinna Maningo ambaye mpaka 

sasa tunapoandika tamko hilo ni siku ya Nne anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kwa 

kutuhuma za kuandika habari za tuhuma za ulawiti uliomhusisha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa 

Simiyu.

Ndugu Wananchi mbali na matukio hayo ya ukamataji na kufunguliwa kesi wanaharakati 

wanaotumia Uhuru wao wa kujileza,pia yapo matukio ya hivi karibuni ya viongozi wa dini pamoja 

na wanasiasa mfano Mwenyekiti UVCCM Taifa ambao wametaka Serikali kufungia mitandao ya X 

na Istagram kwa kile wanachodai kwamba mitandao hiyo inachochea masuala ya ngono.

Sisi Asasi za Kiraia zinazofanya shughuli za Utetezi wa Haki za Binadamu hususani Haki na Uhuru 

wa Kujieleza ( Freedom of Expression) tunaendelea kutoa masikitiko yetu kwa kitendo cha Jeshi la 

Polisi Mkoa wa Mwanza kuendelea kumshikilia Mwandishi wa Habari Dina Maningo pasipo kumpa 

dhamana wala kumfikisha Mahakama kama sheria inavyoelekeza.na pia tunatoa wito kwa Serikali na 

vyombo vingine vya Usalama kuzingatia Katiba ya nchi inayotoa Haki na Uhuru wa Raia wa nchi 

kutumia na kufurahia Uhuru na Haki za Kujieleza ambao kwetu wanaharakati wa Haki za Binadamu 

ni Haki wezeshi wa HAKI zingine zote

Uhuru wa kujieleza ni Haki iliyo katika Katiba yetu na na Haki za Msingi inayowezesh a Haki zingine 

kupatikana ,hivyo vitendo hivi vya Polisi kukamata ,kutisha na kufungulia Waandishi wa 

Habari,Wanaharakati mbalimbali nchini havikubaliki na tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi kumwachia 

Dina Maningo au wamfikishe Mahakamani .

Mwisho tuwaombe Waandishi wa Habari na Mawakili wajitokeze kupigania haki ya Mwandishi Dina 

Maningo pamoja na kupigania haki za wanaharakati wengine Malisa na Boniface na kuendelea 

kukemea na kupinga kwa nguvu zote matishio na majaribio ya wanasiasa na wengine wasio na nia 

njema na Uhuru wa Kujieleza wanaotaka kuzima na kunyonga Haki na Uhuru huu wa Kujieleza 

kwani Shambulio dhidi ya Mwandishi wa Habari ni Shambulio dhidi ya Haki ya Kujieleza na ni 

shambulio dhidi ya Haki za Binadamu.

Tamko limetolewa na:

1. CIVIC AND LEGAL AID ORGANIZATION (CILAO) 

2. MEDIA DEFENCE INITIATIVE (MDI) 

3. OJADACT 

4. MAIPAC

5. Foundation for Development Organization - FODEO


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI