Header Ads Widget

KUKOSEKANA BARABARA CHANZO CHA VIFO WAJAWAZITO KIIJIJI CHA IKOMBE KYELA , MBEYA.

Wakazi  wa kijiji cha Ikombe kata ya Matema Wilayani Kyela Mkoani Mbeya  wameiomba serikali iwatengenezee barabara kutokana na usafiri pekee wa majini wanaotumia katika ziwa nyasa na kwa sasa kuwa si wa uhakika kwani  wakati mwingine  wanashindwa kusafiri kutokana na dhoruba hivyo baadhi ya wagonjwa wanaohitaji huduma za dharula hupoteza maisha.

Tangu kuanzishwa kwa kijiji hicho mwaka 1976 hakijawahi kuwa na barabara hivyo wananchi hawa  wamepenyeza  ombi kwa serikali kupitia mbunge wao.

Mbunge wa jimbo la Kyela Ally Mlaghila Akatangaza neema kwa wananchi hawa wa kijiji cha Ikombe itakayosaidia kumaliza changamoto ya wanawake kujifungulia njiani  wakielekea kutafuta huduma za kiafya.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI