Header Ads Widget

PUTIN KUANZA MUHULA WAKE WA TANO KAMA RAIS WA URUSI

 


Vladimir Putin anaanza muhula wake wa tano kama rais wa Urusi katika hafla ya kuapishwa kwa kifahari ya Kremlin Jumanne, baada ya kuwaangamiza wapinzani wake wa kisiasa na kuunganisha nguvu zote mikononi mwake.

Akiwa tayari afisini kwa takriban robo karne na kiongozi aliyekaa muda mrefu zaidi wa Kremlin tangu Josef Stalin, muhula mpya wa Putin hautaisha hadi 2030, wakati anastahili kikatiba kugombea kwa miaka mingine sita.

Kufuatia kuanza kwa vita na Ukraine mwaka 2022 ambao umekuwa mzozo mkubwa zaidi barani Ulaya tangu Vita vya Kidunia vya pili, Urusi imewekewa vikwazo vikali na nchi za Magharibi na inazielekeza nchi nyingine kama China, Iran na Korea Kaskazini kuungwa mkono.

Swali sasa ni nini Putin mwenye umri wa miaka 71 atafanya katika kipindi cha miaka sita mingine, ndani na nje ya nchi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS