Serikali imetenga jumla ya Shilingi Trillion 1.15 kwa ajili ya kujenga shule mpya za msingi na madarasa mapya kwa kipindi cha miaka 5 ambapo kwa mwaka huu wa fedha Shule 302 mpya za msingi na madarasa zaidi ya 3000 zimejengwa.
Naibu Katibu Mkuu wa Tamisemi (Elimu) Dkt. Charles Msonde amesema hayo wakati akifungua Juma la Elimu Kitaifa wa mwaka 2024 ( GAWE) Mjini Geita na Serikali imefanya hivyo kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundisha.
Dkt. Msonde amesema katika jitihada za kuboresha elimu na miundombinu yake ambapo kwa upande wa shule za sekondari jumla ya Shilingi Trillion 1.2 zimetengwa kwa ajili ya kujenga shule mpya za sekondari 1026 na Kati ya hizo shule 26 zimetengwa mahususi kwa ajili ya wasichana za Mikoa za Bweni.
0 Comments