Header Ads Widget

DEREVA ALIYESABABISHA VIFO VYA WATU SABA ATIWA MBARONI MORO

 


Na Ashton Balaigwa,MOROGORO

JESHI la Polisi mkoani Morogoro limefanikiwa kuwatia mbaroni madereva 10 kwa tuhuma za makosa ya usalama barabarani  akiwemo  dereva wa Lori ,Samsoni Uwiringiyimana (35), raia wa  Rwanda  anayetuhumiwa kwenye  tukio la ajali iliyosababisha vifo vya watu saba na kujeruhi wengine sita iliyotokea siku ya Jumanne wiki hii.


Kamanda wa Polisi wa mkoa  huo , Alex Mkama amesema   kuwa madereva hao wamekakatwa katika operesheni za usalama barabarani zinaendelea kufanyika mkoani Morogoro.

 

Mkama amesema  Samsoni  alikuwa akiendesha gari la mizigo  aina ya MAN lenye  namba za usajili RS 980 X3  ambalo liligongana  uso kwa uso na  gari ndogo ya abiria aina ya Noah yenye namba za usajili T 101 DKB.


Amesema  tukio hilo lilitokea  Mei 14,mwaka huu (2024) ,majira ya saa mbili na nusu asubuhi eneo la Dakawa , wilaya ya Mvomero  wakati gari hilo dogo la abiria ikiwa inatokea  Mji wa Dumila ,wilayani Kilosa kuelekea Morogoro mjini, na  Lori  hilo  la masafa marefu ililikuwa linatokea Morogoro mjini  kwenda Dodoma.


Kamanda huyo wa Polisi wa mkoa  alieleza ya kwamba  baada ya kutokea kwa ajali hiyo Dereva wa Lori alilimbia kusikojulikana  na kulitelekeza gari lake na  kwamba  Polisi  waliazisha msako wa kumtafuta  ili atakapopatikana  aweze kuchukuliwa  hatua za kisheria  na kufikishwa mahakamani. 

MWISHO.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI