Mkuu wa wilaya Same Kasilda Mgeni kushoto,akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka Kwa Mkuu wa wilaya ya Mwanga,Mkoani Kilimanjaro .
Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 umepokelewa wilayani Same , baada ya kumaliza mbio zake kwenye wilaya ya Mwanga makabidhiano yamefanyika viwanja vya shule ya Msingi Njoro halmashauri ya Wilaya ya Same.
Mkuu wa Wilaya ya Same Kasilda Mgeni amepokea mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Abdallah Mwaipaya akisema ukiwa wilayani humo utakimbizwa umbali wa KM 138.4 kutembelea, kuweka Mawe ya Msingi na kuzindua jumla ya miradi Nane (8) yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 3.6.
Wilaya ya Same inakua wilaya ya Saba kwenye mkoanwa Kilimanjaro na ndio itahitimisha mbio ni hizo kimkoa kwa mwaka huu 2024, kisha kukabidhi mkoa jirani wa Tanga hapo kesho Aprili 9,mwaka huu 2024.
Mwisho
0 Comments