Header Ads Widget

MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA YABADILI TASWIRA, SEKTA YA KILIMO JIJI LA DODOMA



Na John Masanja:

Miaka 3 ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt, Samia Suluhu

Hassan imetajwa kuleta mabadiliko chanya katika eneo la kilimo ndani ya Jiji la

Dodoma kupitia matokeo makubwa yanayothibitishwa na wakulima, wafugaji pamoja na

wasimamizi wa masuala ya kilimo.

Akizungumza na vyombo vya habari Mkuu wa Divisheni ya Kilimo Mjini, Yustina

Munishi alisema kwa kipindi cha Miaka 3 ya serikali ya Awamu ya Sita, Jiji la Dodoma

limepiga hatua kubwa katika eneo la kilimo kutokana na uzalisahaji mkubwa wa mazao

ya chakula, mazao ya kibiashara halikadhalika ongezeko la mifugo.

Aidha, kupitia mazungumzo yake alisema “Serikali imekuwa na mchango mkubwa

kuyafikia mafanikio haya, kwakuwa wamekuwa kipaumbele kutoa fedha, usimamizi

mzuri, elimu kwa wakulima na watumishi, hii yote ni kuhakikisha kilimo cha Jiji letu

kinastawi siku hadi siku”

Munishi aliyataja na kuyafafanua maeneo mbalimbali katika Divisheni yake ambayo

yamekuwa na mafanikio yaliyotukuka kwa kipindi cha miaka 3.

Alisema zao la zabibu limekuwa ni moja ya zao la kimkakati ambalo linalimwa zaidi na

kwa mafanikio makubwa hadi sasa ndani ya Jiji la Dodoma kupitia msukumo na

hamasa iliyofanyika ikiwa ni pamoja na mafunzo mbalimnbali yaliyotolewa kwa

wakulima na watumishi kuhusiana na uzalishaji mzuri na wenye tija.

“Tumeongeza uzalishaji wa zao la Zabibu miche 113,306. Hadi sasa wakulima 500 na

watumishi 30 wameweza kupata mafunzo kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa

Kilimo Tanzania – Makutopora” alisema Munishi.

Aidha alisema kumekuwa naongezeko la viwanda zaidi ya 20 ambavyo vinaboresha na

kuongeza thamani ya zao la zabibu, ikiwa ni mafanikio waliyoyapata ndani ya miaka mi

tatu ya serikali ya awamu ya sita.

Sambamba na hayo alisema serikali imewasaidia kuboresha huduma za ugani kwa

kuwapatia vitendea kazi ikiwa ni pamoja na jumla ya pikipiki 28. Alisema pikipiki hizo

zimekuwa na msaada mkubwa katika kuboresha na kurahisisha huduma, kwakuwa

wakulima wengi wanafikiwa na kupata huduma za ugani na teknolojia mbalimbali, hali

inayopelekea ongezeko kubwa la uzalishaji wa chakula.

Hata hivyo alisema kwa kipindi cha miaka mitatu ya Rais. Dakt, Samia Suluhu Hassan,

divisheni ya kilimo mjini kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, wamehakikisha mbegu

ya alizeti ya ruzuku imetolewa kwa wakulima wote hadi wa ngazi ya Kata kwa bei nafuu.

“tumefanikiwa kununua na kusambaza mbegu ya alizeti ya ruzuku tani 45,000 zenye

thamani ya shilingi milioni 225 na kuziuza kwa wakulima kwa bei ya shilingi 5,000 kwa


kilo hali iliyowezesha kushuka kwa gharama ya mafuta ya alizeti kutoka (6,000 – 7,000)

kwa lita hadi sasa kufikia (4,000 – 5,000)” alisema Munishi.

Aidha alisema fanikio jingine walilolipata ni kusajili jumla ya wakulima 14,430 ambao pia

wameweza kupatiwa huduma ya kununua mbolea ya ruzuku.

“Awamu hii tumeweza kupata dozi 4,000 za madume bora ambayo yanapandishwa kwa

mitamba yetu na kuboresha uzalishaji kwa njia ya mirija” aliongezea Munishi na kusema

kuwa, kupitia teknolojia hiyo imepelekea ongezeko la maziwa na ngombe ambapo hadi

kufikia sasa mmfugaji mmoja anaweza kupata maziwa lita 20 - 30 kwa siku.

Aidha alisema kupitia ufugaji wa kuku, Divisheni ya kilimo Mjini ndani ya miaka mi tatu

ya Serikali ya Awamu ya Sita imeweza kupunguza vifo vya kuku kutoka asilimia 5

mpaka 3 kupitia utoaji wa chanjo uliofanyika.

Hata hivyo, alisema wamefanikiwa kuboresha miundombinu ya mifugo kwa kiasi

kikubwa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa wigo katika minada mbalimbali hali ambayo

imesaidia kuhakikisha usalama wa mifugo isitoroshwe lakini pia kuondo mianya ya

upotevu wa ukusanyaji wa mapato kwenye maeneo hayo.

Sambamba na hilo alisema eneo la Ipala wamefanikiwa kutengeneza bwawa la

kunyweshea mifugo linalowanufaisha zaidi ya wafugaji 1865 kwa Kata moja na pia

wananendelea kuboresha kwenye maeneo mengine yanayofaa kwaajili ya kutengeneza

mabirika hayo.

Aidha, alisema kwa kipindi cha miaka mi tatu cha Serikali ya Awamu ya Sita

wamefanikiwa kuchanja Ng’ombe 64,000, Mbuzi na Kondoo 52,340 kwa gharama nafuu

ya ruzuku.

“Divisheni yetu ipo kwa ajili ya kuwapa watu furaha na Lishe bora kwa sababu watu

wasipokula hawawezi kuwa na furaha. Watu wasipopata kuku na vitoweo kama nyama

ya ng’ombe hawawezi kupata furaha” Munishi aliongezea.

Kwa upande mwingine Munishi alisema kwa kipindi cha miaka mitatu halmashauri ya

Jiji imekuwa washindi wa kwanza kimkoa katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati

kwa mwaka 2023.

Munishi alihitimisha kwa kutoa shukurani pangezi za dhati kwa Rais. Mhe, Samia

Suluhu Hassan kwa kuboresha shughuli za kilimo katika Jiji la Dodoma na kuahidi

kuendelea kuunga mkono jitihada zake katika kuwaletea wanancghi maendeleo.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI