Shirika
la Sauti ya Haki Tanzania limetoa mitaji ya fedha kwa wanawake 10 wakazi wa mtaa
wa Mibata kata ya Nduli, manispaa ya Iringa, ambao wanajishughulisha na kazi ya
kupika na kuza pombe za kienyeji ili kulea familia zao, lengo likiwa ni kuwezesha
wanawake hao kufanyabiashara nyingine za kiuchumi na kupata muda kulea familia
zao ili kupunguza udumavu na ukatili kwa Watoto .
Akizungumza
katika hafla ya kukabidhi fedha hizo, Mkurugenzi wa sauti ya haki Tanzania,
Wakili Leticia Petro Ntagazwa, amesema matumizi ya pombe za kienyeji ndani ya
mkoa wa Iringa yamezidi kushika kasi jambo ambalo linaathiri makuzi na usalama
kwa Watoto, jambo ambalo linachangia Watoto wengi kukataa shule na kujiingiza
katika matumizi ya pombe wakiwa na umri mdogo.
Amesema,
anaamini Mitaji hiyo itakwenda kubadilisha Maisha ya wanawake hao kwa kuanzisha
biashara mbadala na uuzaji wa Pombe za Kienyeji, jambo ambalo litawezesha kuwa
na muda wa kulea familia zao vyema.
Aidha
Waikili Letiaci Petro Ntagazwa, amewakumbusha wanaume kusimamia majukumu yao ya
kulea familia ili kupunguza wimbi la Watoto wanaopitia changamoto za ukatili
kutokana na wanawake kuachiwa majukumu yote hivyo kukosa muda wa kuangalia Watoto
wao.
Katika
hatua nyingine amewakumbusha wazazi na walezi kuwa natabia ya kuzungumza na Watoto
wao mara kwa mara ili kuweza kutambua changamoto wanazozipitia hasa pindi
wanapokuwa mbali nao, kwani itasaidia kupunguza ukatili kwa Watoto.
Naye
Afisa kutoka mamlaka ya kudhibiti na
kupambana na dawa za kulevya kanda ya Nyanda za juu kusini, Adrick Simon Ndelwa,
amesema kwa sasa wafanyabiashara wa dawa za kulevya wamekuja na mbinu mpya za
kusafirisha dawa hizo kwa kutumia vyakula kama biscuit, cake na vyakula vingine
jambo ambalo linafanya kufikiwa na kutumiwa na Watoto wadogo, hivyo kuwataka
wazazi na walezi kuwa makini na Watoto wao kwa kuwaonya juu ya kupokea vitu
kutoka kwa watu wasio wafahamu.
Kwa
upande wao wananchi walioshiriki sherehe hizo wamelishukuru shirika hilo kwa
kuendelea kuwasaidia wakazi waneo hilo katika Nyanja mbalimbali hasa ushauri wa
kisheri Pamoja na elimu za ujasiriamali.
Prisca
Lameck, mkazi wa mtaa wa Mibata kata ya Nduli, amesema tatizo kubwa linalo
wakabili Watoto wa eneo hilo ni wazazi wao kushinda vilabuni kutokana na kufanyabiashara
ya pombe za kienyeji au kuwa wanywaji wa pombe hizo hivyo kupelekea Watoto wengi
kuingia kwenye makundi hatari kutokana na kukosa maelezi ya wazazi.
Naye
Diwani wa kata ya Nduli Bashiru Mtove, amelishukuru shirika la sauti ya haki
Tanzania kwa kuendelea kuisaidia jamii kwa kutoa elimu Pamoja na mitaji ya
biashara kwani jambo hilo limekuwa na msaada mkubwa sana kwa watanzani.
Shirika
la sauti ya haki Tanzania limeanzishwa mwaka 2016 lengo likiwa ni kulinda,
kutetea na kuhamasisha haki za wanawake na Watoto na kwa sasa linafanya kazi
mbalimbali kama elimu ya haki za wanawake na Watoto, msaada wa kisheria, elimu
ya ukatili wa kijinsia, elimu ya mazingira na kutunza mazingira, elimu ya
kijinsia na ya mabadiliko ya tabia nchi Pamoja na kuwawezesha wanawake kiuchumi
kwa kuwapatia miradi mbalimbali kama vile ufugaji wanyuki, na mikopo midogo midogo
kwa wanachama.
0 Comments