Jumla ya watuhumiwa 12 akiwemo mfanyabiashara Ghulam Rasoul Abrahimu Mia wamefikishwa Mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya mkoa wa Iringa kwa tuhuma 6 ikiwemo ya uhujumu Uchumi na utakatishaji fedha kwa kujipatia lita za mafuta aina ya Disel lita laki saba na Hamsini na tatu zenye thamani ya kiasi cha shilingi bilioni mbili nukta mbili.
Watuhumiwa hao 12 walifikishwa jana mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya mkoa wa Iringa Hororius kando wakisomewa makosa 6 huku kosa moja la utakatishaji pesa kwa kujipatia mafuta aina ya disel lita 705,300 zenye thamani ya Tsh bilioni 2,292,075,944.60 ambapo watuhumiwa hao wakabiliwa na kesi ya uhujumu Uchumi namba 5001 ya mwaka 2024.
Kosa la kwanza walilosomewa wote ni kuongoza gege la uhalifu kinyume na kifungu namba 57 na kifungu namba 60 cha sheria ya uhujumu Uchumi wakati kosa la pili uharibifu wa mali kinyume na kifungu namba 326 cha sheria ya makosa ya jinai .
Huku kosa namba 3 ni wizi kinyume na kifungu namba 258 na 255 cha sheria ya makosa ya jinai na kosa la nne ni kuisababishia hasara mamlaka kinyume na na kifungu cha 57 na 60 ya sheria ya uhujumu Uchumi huku kosa la sita ni utakatishaji wa pesa .
Upande wa washtakiwa wanatetewa na mawakili watatu akiwemo Barnabas Nyalusi, Moses Ambwindwile na Stanley Nyamley huku upande wa jamhuri kukiwa na mawakili watatu .
Kesi hiyo itatajwa tena March 25 mwaka huu na watuhumiwa hawakutakiwa kujibu chochote na kurudishwa mahabusu, kwa kuwa mahakama hiyo haina nguvu kisheria .
……………
0 Comments