Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
WANAOPISHA UWANJA WA NDEGE KIGOMA WALIA FIDIA KUCHELEWA
WANAOPISHA UWANJA WA NDEGE KIGOMA WALIA FIDIA KUCHELEWA
Misalaba
Tuesday, February 13, 2024
Fadhili Mayogela mmoja wa wakazi wa manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye nyumba yake inavunjwa na kulipwa fidia kupisha mradi wa upanuzi wa uwanja wa ndege kigoma
Na Fadhili Abdallah,Kigoma
WAKAZI 360 kutoka kata tatu za manispaa za manispaa ya Kigoma Ujiji wanaopisha maeneo yao kwa ajiili ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma wameiomba serikali kuharakisha kulipa fidia ya maeneo kutokana na adha kubwa wanayopata sasa baada ya kuzuiwa kutofanya chochote kwenye maeneo hayo kwa sasa.
Wakizungumza na waandishi wa Habari mjini Kigoma wananchi hao walisema kuwa wakati huu wa mvua nyingi wanapata adha kubwa ikiwemo kuanguka kwa nyumba zao lakini maji kuibuka ndani ya nyumba kama chemchem adha ni kubwa kwao ni bora walipwe watafute la kufanya.
Mmoja wa wananchi hao, Fadhili Hamisi Mayogela kutoka kata ya Machinjioni Ujiji mjini Kigoma alisema kuwa tangu mwezi Machi mwaka jana walizuiwa kutofanya chochote kwenye nyumba hizo kwa maana watalipwa fidia ndani ya miezi sita lakini hakuna kilichofanyika.
Kufuatia hali hiyo mwananchi mwingine Salama Ramadhani Bilali amemuomba Raisi Samia Suluhu Hassan aingilie kati suala hilo kutokana na sintofahamu inayokumba na kwamba kama serikali haina pesa za kulipa kwa sasa iwaruhusu wafanyie ukarabati nyumba zao na fidia ifanyike upya watakapopata fedha za kulipa.
Akizungumzia hali hiyo Mkuu wa mkoa Kigoma,Thobias Andengenye amekiri kuwepo kwa mpango wa fidia kwa wananchi wa kata tatu za manispaa ya Kigoma Ujiji ambao wanapaswa kuondoka maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma.
Mkuu huyo wa mkoa amekiri kuchelewa kufanyika kwa malipo hayo ingawa amebainisha kwamba serikali inafanya juhudi kuhakikisha malipo hayo yanafanyika ili malipo ya fidia yasiwe kikwazo kwa utekelezaji wa mradi huo ambao tayari umeshaanza.
Baadhi ya nyumba za kata ya kitongoni manispaa ya Kigoma Ujiji ambazo zitavunjwa na kulipwa fidia kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
TUZIDI KUUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS SAMIA KATIKA KUDUMISHA AMANI YETU – JASMIN NG’UMBI
Gasper
Friday, July 11, 2025
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan NA MATUKIO DAIMA MEDIA MUFINDI Kada wa Chama Cha Mapi…
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
WALIOSOMA SHULE YA MSINGI MITWERO WAIPIGA JEKI SHULE MADAWATI
Friday, July 04, 2025
WANAWAKE MORO WAAMKA KWA KISHINDO KUCHUKUA FOMU ZA UDIWANI
Friday, July 04, 2025
NAFASI ZA KAZI NEC UCHAGUZI MKUU 2025
Friday, April 04, 2025
Contact form
0 Comments