Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
WANAOPISHA UWANJA WA NDEGE KIGOMA WALIA FIDIA KUCHELEWA
WANAOPISHA UWANJA WA NDEGE KIGOMA WALIA FIDIA KUCHELEWA
Misalaba
Tuesday, February 13, 2024
Fadhili Mayogela mmoja wa wakazi wa manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye nyumba yake inavunjwa na kulipwa fidia kupisha mradi wa upanuzi wa uwanja wa ndege kigoma
Na Fadhili Abdallah,Kigoma
WAKAZI 360 kutoka kata tatu za manispaa za manispaa ya Kigoma Ujiji wanaopisha maeneo yao kwa ajiili ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma wameiomba serikali kuharakisha kulipa fidia ya maeneo kutokana na adha kubwa wanayopata sasa baada ya kuzuiwa kutofanya chochote kwenye maeneo hayo kwa sasa.
Wakizungumza na waandishi wa Habari mjini Kigoma wananchi hao walisema kuwa wakati huu wa mvua nyingi wanapata adha kubwa ikiwemo kuanguka kwa nyumba zao lakini maji kuibuka ndani ya nyumba kama chemchem adha ni kubwa kwao ni bora walipwe watafute la kufanya.
Mmoja wa wananchi hao, Fadhili Hamisi Mayogela kutoka kata ya Machinjioni Ujiji mjini Kigoma alisema kuwa tangu mwezi Machi mwaka jana walizuiwa kutofanya chochote kwenye nyumba hizo kwa maana watalipwa fidia ndani ya miezi sita lakini hakuna kilichofanyika.
Kufuatia hali hiyo mwananchi mwingine Salama Ramadhani Bilali amemuomba Raisi Samia Suluhu Hassan aingilie kati suala hilo kutokana na sintofahamu inayokumba na kwamba kama serikali haina pesa za kulipa kwa sasa iwaruhusu wafanyie ukarabati nyumba zao na fidia ifanyike upya watakapopata fedha za kulipa.
Akizungumzia hali hiyo Mkuu wa mkoa Kigoma,Thobias Andengenye amekiri kuwepo kwa mpango wa fidia kwa wananchi wa kata tatu za manispaa ya Kigoma Ujiji ambao wanapaswa kuondoka maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma.
Mkuu huyo wa mkoa amekiri kuchelewa kufanyika kwa malipo hayo ingawa amebainisha kwamba serikali inafanya juhudi kuhakikisha malipo hayo yanafanyika ili malipo ya fidia yasiwe kikwazo kwa utekelezaji wa mradi huo ambao tayari umeshaanza.
Baadhi ya nyumba za kata ya kitongoni manispaa ya Kigoma Ujiji ambazo zitavunjwa na kulipwa fidia kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
SERIKALI YATANGAZA BEI YA PAMBA HUKU IKITOA MAELEKEZO.
BARIADI NEWS
Friday, May 02, 2025
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Kenan Kihongosi (mwenye tai) akishuhudia zoezi la Uzinduzi wa …
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
BREAKING:DKT KITIMA AJERUHIWA NA WATU WASIOJULIKANA
Thursday, May 01, 2025
WANANCHI ULYANKULU WAMPA KONGOLE RAIS SAMIA ZOEZI LA MADAKTARI BINGWA
Thursday, May 01, 2025
WAMECHUKUA VYOMBO VYANGU VYOTE VYA NDANI KISA MADENI -SIMULIZI
Thursday, May 01, 2025
Contact form
0 Comments