Header Ads Widget

WAFANYABIASHARA WAHIMIZWA KUFUATA MAELEKEZO YA SERIKALI JUU YA BEI YA SUKARI.

 

Na SHEMSA MUSSA,KAGERA MULEBA ,

Serikali Wilayani Muleba Mkoani Kagera imewasisitiza Wafanyabiashara  kuendelea kutekeleza na kufuata   maelekezo ya Serikali kuhusiana na upandaji  wa bei ya Sukari unaoendelea kuwaumiza Wananchi.


Kauli hiyo ilitolewa na Benjamin Mwikasyege ambaye ni katibu Tawala wa Wilaya  Muleba  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya hiyo wakati akitoa maelekezo ya Serikali katika kikao cha Baraza la Madiwani kilicholenga  kujadili taarifa za utekelezaji kwa robo ya pili Oktoba-Desemba 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.


Mwikasyege alisema kuwa katika maeneo mbali mbali sukari imepanda ambapo  wao walivyokubaliana kati ya Serikali ya Wilaya hiyo na Wadau mbali mbali ni kwamba  kilo moja ya Sukari iuzwe kwa kiasi cha  shilingi 3,500  na kuwa katika maeneo mengine sukari imeendelea kuuzwa zaidi ya  kiwango tajwa jambo linalowaumiza Wananchi na kuwa kero.


Aidha Kufuatia hali hiyo ameahidi kuwa Serikali Wilayani humo itaendelea kufuatilia jambo hilo kwa ukaribu sana ili lisiendelee kuwa kero


Hata hivyo aliwasihi madiwani wa Halmashauri hiyo kuendelea kusisitiza suala hilo kwa wafanyabiashara ili bei isizidi kiwango kilichoelekezwa na Serikali.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI