Header Ads Widget

RIDHIWANI KIKWETE APOKEA MSAADA WA SOLA YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 16 KWAAJILI YA SHULE YA SEKONDARI JAKAYA MRISHO KIKWETE HUKO CHALINZE


Na Scolastica Msewa, Chalinze 

Naibu Waziri wa ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chalinze Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete  amepokea na kuzindua Mradi wa Umeme wa Sola katika Shule ya Sekondari ya Jakaya Mrisho Kikwete wenye thamani ya zaidi ya milioni 16 huko Msolwa Chalinze mkoani Pwani msaada uliotolewa na Kampuni ya Matheostechs kwa lengo la kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita katika kuboresha sekta ya elimu nchini.


Mheshimiwa Ridhiwani amepokea na kuzindua Mradi huo wa Umeme wa Sola huko Katika shule mpya ya Jakaya Mrisho Kikwete ambayo imejengwa kwa lengo la kusogeza Shule ya Sekondari kwenye kijiji ambacho walikuwa wakitembea umbali mrefu kufuata shule.

Amesema shule hiyo mpya inayoendelea kujengwa Ina miundombinu mizuri lakini hakukuwa na umeme kwakuwa umeme hajafika katika eneo.hilo lakini kwa ushirikiano wa Kampuni ya Matheostechs wakesaidia kumaliza tatizo Hilo la kukosa Umeme shuleni hapo 


Aidha amewataka Wanafunzi, Walimu na Wazazi kuisaidia kutunza miundombinu mizuri ya mfumo wa 

Umeme huo sambamba na kuwataka Wanafunzi kusoma kwa bidii kwa lengo la kuenzi jina kubwa la Jakaya Mrisho Kikwete.



Awali Mkurugenzi wa Kampuni ya Matheostechs Theobald Bonaventure amesema Kampuni yake iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni kushiriki jitihada za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuboresha sekta ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuenzi jina kubwa la Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuweka Umeme wa Sola kwenye shule hiyo ambayo illihitaji umeme.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI