Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
BENKI KUU YATOA WITO KWA JAMII KUSAJILI VIKUNDI VYA KUWEKA NA KUKOPA
BENKI KUU YATOA WITO KWA JAMII KUSAJILI VIKUNDI VYA KUWEKA NA KUKOPA
Misalaba
Friday, February 16, 2024
NA THABIT MADAI,ZANZIBAR
BENKI Kuu ya Tanzania imetoa wito kwa jamii kuwa na muamko wa kusajili vikundi vya kuweka na kukopeshana Fedha katika maeneo mbalimbali nchini ili kuepuka hasara ambazo zinazoweza kupatikana wakiwa wanasimamia vikundi vyao kienyeji.
Wito huo umetolewa na Afisa Mkuu Mwandamizi kutoka Idara ya Usimamizi wa huduma ndogo za Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Deogratias Mnyamani katika siku ya pili ya mafunzo kwa Wahariri wa Vyombo mbalimbali vya Habari yanaondeshwa katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya BoT Zanzibar.
Amesema kwamba, Kuna faida nyingi za kusajili vikundi ikiwemo kutambulika rasmi kisheria sambamba na usalama wa Fedha za Wanachama unakuwa Mkubwa zaidi.
"Unaposajili hivi vikundi vya kuweka na kukopeshana fedha zinakuwa katika usalama Mkubwa zaidi wa fedha za Wananchama na hata Kesi zinapungua katika jamii yetu," ameeleza.
"Nichukue nafasi hii kuwashauri wote ambao wamejiunga katika vikundi ambavyo havijasajiliwa wajitokeze kusajili ili kupata faida zaidi," ameongeza.
Katika hatua nyingine ameomba Waandishi wa Habari kuendelea kutoa Elimu kwa jamii juu ya kusajili vikundi vya kukopeshana fedha ili kuokoa hasara ambayo wanajamii wanaweza kuipata.
"Tunategemea kuwa nyinyi Waandishi wa Habari mutaendelea kutoaelimu kwa jamii ili kuepuka hasara ambayo inaweza kujitokeza,"Ameeleza.
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
magazeti
MEZA YA MAGAZETI JUMATANO JUNI 25/2025::MAKONDA SASA RASMI KUTIFUABA NA MRISHO GAMBO ARUSHA MJINI,GRACE TWNDEGA ATAJWA UBUNGE KALENGA
Gasper
Tuesday, June 24, 2025
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
BREAKING:RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI HUU ,KHERI JAMES AWA MKUU WA MKOA WA IRINGA ,KENANI KIHONGOSI MKUU WA MKOA ARUSHA
Monday, June 23, 2025
MAFUNZO MAALUMU KWA WALIMU WA SOMO LA BIASHARA NA AMALI YAENDELEA KOROGWE
Monday, June 23, 2025
RAIS AKUBALI OMBI LA PETER SERUKAMBA KWENDA KUTIA NIA UBUNGE
Monday, June 23, 2025
Contact form
0 Comments