Na Hadija Omary
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso ameiweka katika uangalizi wa mwezi mmoja Bodi ya Mamlaka ya Maji mjini Lindi (LUWASA) kutokana na kutotekeleza majukumu yake ipasavyo yakufuatilia na kusimamia utendaji kazi wa mamlaka hiyo.
Ametoa kauli hiyo leo januari 26,2024 wakati anazungumza na bodi ,watumishi wa mamlaka hiyo pamoja watumishi kutoka wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini Ruwasa Mkoa wa Lindi.
Hata hivyo Waziri Aweso ameahidi kuleta timu itakayowasaidia huku akiweka bayana maamuzi atakayoyaamua ya kuivunja bodi hiyo endapo haitofanya kazi yake ya kuisaidia mamlaka kwa kuwasimamia watumishi kufanya kazi kwa weledi na kuboresha huduma .
Aweso pia aliisisitiza bodi hiyo kutimiza majukumu yake ikiwemo kufuatilia utendaji kazi wa watumishi wa mamlaka jambo litakosaidia kuboreshahali ya upatikanaji wa huduma na kufanya kazi vizuri kama mamlaka zingine za maji kutoa huduma bora kwa wananchi.
0 Comments