Nyota wa
"Fast & Furious" Vin Diesel anashutumiwa kwa unyanyasaji wa kingono
na msaidizi wa zamani.
Katika kesi
iliyowasilishwa Los Angeles Alhamisi, Asta Jonasson anadai kuwa mwigizaji huyo
alimnyanyasa kijinsia msimu wa 2010 wakati wa kurekodi filamu ya "Fast
Five" huko Atlanta.
Kwa mujibu
wa kesi hiyo, Jonasson aliajiriwa na kampuni ya utayarishaji filamu ya
muigizaji huyo ya One Race ili kumfanyia kazi mbalimbali, ikiwa ni
pamoja na kuandaa na kumsindikiza Diesel kwenye tafrija na kuhakikisha yuko
karibu kwenye picha ikiwa mwigizaji huyo alihudhuria hafla bila mpenzi wake wa
muda mrefu.
Wakili
kutoka Greenberg Gross, kampuni inayomwakilisha Jonasson, alisema katika
taarifa yake: "Tunajivunia kumwakilisha Bi. Jonasson na kumwajibisha Vin
Diesel na wale walioruhusu na kuficha unyanyasaji wake wa kijinsia. Sheria ipo
kuwalinda wale ambao wamekuwa wakidhulumiwa, haijalishi mshtakiwa ana nguvu au
umaarufu kiasi gani. Unyanyasaji wa kijinsia mahali pa kazi hautakoma kamwe
ikiwa wanaume wenye nguvu watalindwa dhidi ya uwajibikaji."
Bryan
Freedman, wakili wa Los Angeles anayemwakilisha Vin Diesel, alisema katika
taarifa kwamba Diesel "anakanusha madai hayo yote kwa ukamilifu."
"Hii ni
mara ya kwanza kwake kusikia kuhusu madai hayo ya zaidi ya miaka 13
yaliyotolewa na mfanyakazi anayedaiwa kuwa wa siku 9," Freedman alisema
katika taarifa hiyo. "Kuna ushahidi wa wazi ambao unakanusha kabisa madai
haya ya ajabu."
Madai hayo
yanaeleza kuwa baada ya usiku wa Septemba 2010, Jonasson aliombwa kumsubiri
Diesel, 56, katika chumba chake ndani ya hoteli ya St. Regis, Diesel alishika viganja vya Jonasson na kumvuta kitandani,
kwa mujibu wa kesi hiyo.
Alimuonya na
kumtaka Diesel aondoke, lakini inadaiwa alianza kupapasa matiti yake, kumbusu
kifuani na kumshika kiunoni na juu ya miguu yake, yakiwemo mapaja ya ndani.
Jonasson
aliogopa "kumzuia mkuu wake" kwa usalama wake binafsi na usalama wa
kazi, lakini baada ya Diesel kusogea kushusha chupi yake, Jonasson alipiga
mayowe na kukimbia.
Kulingana na
kesi hiyo, Diesel alimbana ukutani na kuweka mkono wake kwenye sehemu zake za
siri. Alipiga punyeto, huku "akiwa na hofu, Bi. Jonasson alifumba macho,
akijaribu kujitenga na unyanyasaji wa kijinsia na kuepuka kumkasirisha,"
kulingana na kesi hiyo.
Saa chache
baadaye, dadake Diesel na rais wa One
Race Samantha
Vincent alimpigia Jonasson kumfukuza kazi baada ya kukaa kazini kwa muda usizidi
wiki mbili kazini, shauri hilo linasema.
Chanzo; USA
TODAY
0 Comments