Header Ads Widget

MACHA:TUNZENI SIRI ZA VIKAO VYA CHAMA

 

NA HAMIDA RAMADHANI, MATUKIO DAIMA AAP DODOMA

KAIMU Katibu Mkuu wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara Anamringi Macha amewataka  Wajumbe wa Jumuiya ya wazazi kutunza siri za vikao vya Chama lengo likiwa ni kuendelea kukilinda Chama na taifa Kwa ujumla. 


Macha  ameyasema hayo leo Desemba 6, 2023 Jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha Baraza kuu la Jumuiya ya wazazi Chama cha Pinduzi CCM.


Amesema katika vitu ambavyo vinaweza kuharibu mustakabari wa Chama ni pamoja na wajumbe kutokuwa na Siri ya yale yote yanayoelekezwa na kukubaliana nadani ya vikao vya chama.

" Niwaombe tutunze Siri za vikao vyetu vya chama pindi tunapokutana na kufanya vikao vyetu ili kukilinda chama Chetu Cha Mapinduzi  na Taifa la Tanazania kwa ujumla,"amesema Macha 


Aidha akizungumzia suala la maadili amesema ili kukemea maadili mabovu kwa vijana ni wazi sasa kama wazazi kutafakari mienendo yao kama inafaa   ili kuweza kuwasaidia vijana  na jamii Kwa ujumla.


Hata hivyo amewataka baadhi ya watu wanaotumika kuivuruga jumuiya hiyo kuacha mara moja  jambo hilo kwa kuwa ni la aibu .


 "Badala yake fanyeni kazi Kwa kufuata kanuni , Taratibu huku mkivumiliana, kupendana na Kwa ushirikiano ili  kuijenga imara jumuiya  na Chama kwa ujumla," amesema .


Amesema ili jumuiya hiyo irudi katika ubora wake ni wakati sasa wakuongeza juhudi,  nakufanyakazi kwa kupendana , Kuvumiliana na kwa kushirikiana

" Tutumie vikao kujadili mambo yetu, kama Kuna watu wachache wapo kwaajili ya kuivuruga jumuiya hii tusiwape nafasi na tukishindwa kufanyakazi Kwa Kuvumiliana basi tufuate kanuni  ," ameeleza  Macha. 


Na kuongeza kusema"  Na sisi kama Chama  hatutokubali kuanza kufikiriana fikiriana , tutafute mambo ya msingi kuijenga jumuiya tusianze chokochoko, " amesema Macha.


Naye Makamu  Mwenyekiti wa jumuiya  hiyo Dogo Iddi Mabrouk ameendelea kusisitiza juu ya utunzaji  wa siri nakuwataka wajumbe hao kuacha mambo ya kitoto nawafanye mambo kama watu wazima.


Katika hatua nyingine  mwenyekiti wa  jumuiya hiyo Fadhil Maganya  amesema jumuiya hiyo imesikitishwa na maafa yaliyotokea katika Kijiji cha Katesh Wilaya ya Hanang Mkoa wa Manyara kufuatia vifo na watu wengine kujeruhiwa kutokana na kunyesha Kwa mvua na  kusababisha mafuriko ya matope na kusema kama jumuiya  desemba 6, 2023  itaungana na viongozi wengine kutoa pole na faraja ikiwemo bidhaa za chakula  Kwa wahanga hao.


Kikao hicho Cha Baraza Kuu la Jumuiya ya wazazi ni cha siku moja na kimehudhuriwa na wajumbe 109 kati  ya wajumbe halali 145.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI