Header Ads Widget

BARAZA LA MAASKOFU LATOA POLE KWA RAIS DKT SAMIA

 



Na Matukio Daima Media ,Mbeya

RAIS wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mbeya Mhashamu ,Gervas Nyaisonga amesema  wamesikitishwa na maafa makubwa ya maporomoko ya udongo  yaliyotokea mlima Hanang Mkoa wa  Manyara ambayo yameathiri  mji mdogo wa Katesh  na kusababisha vifo vya watu 65  na kaya zaidi  ya 1,150 kuathiriwa vibaya,


Katika maafa hayo yamepelekea watu 5,600  kuathirika na  mafuriko huku  wengi  wao walionusurika  wakiwa  wamehifadhiwa kwenye majengo ya Kanisa,Shule na kwa watu wengine wenye mapenzi mema .



 Mhashamu Baba Askofu Nyaisonga  ametoa kauli hiyo leo Jumatano ,Desemba 6,2023  kwa niaba ya baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania  (TEC)  wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Jimbo Kuu la Mbeya kuhusiana na maafa  hayo makubwa kwa taifa.


“Hili ni tukio baya la maafa makubwa ambayo yanasikitisha  tunatoa pole kwa  wananchi  wote wa  Hanang  na Mkoa mzima  wa Manyara ,watanzania wote pia kwa  Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan na tunakiri maafa haya  yana mguso wa kimazingira  yasiyo epukika kwa udharura wa papo kwa papo “amesema.


Ameongeza kuwa “Tunakiri  kuwa  maafa haya yamesababisha vifo vingi  na upotevu wa mali  pamoja na uharibifu wa miundo mbinu na kupelekea usumbufu  mkubwa wa watu , kikubwa tuishukuru  serikali kwa hatua  za dharura  walizochukua , wanajeshi askari wetu, na watu wote waliojituma kushughulikia uokoaji wa haraka kwa watu walioathirika”amesema  Mhashamu Baba Askofu Nyaisonga.


Aidha Askofu Nyaisonga amewatia moyo walioathiriwa na maafa hayo  na kuwashukuru wale wote waliotoa msaada huku akiwataka watanzania wote kutokata tamaa kwa kuwa wakalimu kwa wananchi waliokutwa na maafa hayo makubwa  waendelee kumwamini Mungu kuwa anawapenda na kuwapa ujasiri pamoja na kuendelea kuwaombea majeruhi wote.


Akizungumzia kuhusu msaada kwa waathirika Askofu Nyaisonga amesema kuwa tayari wameanza kuratibu utaratibu wa kupeleka msaada kupitia kitengo cha Caritas kinachoshughulikia maafa ikiwepo   Dawa , vyakula , mavazi na mbegu za mashamba  tayari waraka umesaniwa kwa ajili ya kukabidhi vitu hivyo .


“Huo sio  mwisho wanaendelea kuwasiliana na wahisani wao ndani na nje ya nchi pamoja na washirika ili kuendelea kutoa misaada.


Aidha amesema kuwa kwa upande wa baraza la maaskofu wanaendelea kuratibu kupitia kitengo cha maafa cha CARITAS na kuhamisha kwenyemajimbo kuchangia misaada hiyo .


 


Mwisho.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI