Header Ads Widget

WAKALA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE MBARONI KWA KUGHUSHI

 

Steven Meo Mwasumilwe ambaye ni Wakala wa kukusanya ushuru Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kughushi .

Mtuhumiwa huyo amefikishwa  Octoba 30 mwaka huu katika  Mahakama ya Wilaya Rungwe, mbele ya  Hakimu Mwinjuma Bakari Banga .


Katika kesi hiyo  ya uhujumu uchumi namba 04/2023, Jamhuri dhidi mtuhumiwa  huyo ameshtakiwa kwa kosa la kugushi stakabadhi  zenye  kiasi cha Sh. 330,000/= mali ya Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe.


Ilidaiwa kuwa  Bwana Mwasumilwe alikusanya fedha za Ushuru wa Mazao na kufuja fedha hizo Kwa kutoa stakabadhi za kugushi  baada ya hapo alizitumia  fedha hizo  kwa matumizi yake binafsi. 

Kosa hili ni kinyume na kifungu cha 335(a) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16(RE: 2022)

Mshtakiwa baada ya kusomewa mashtaka yake amerudishwa rumande baada ya kukosa dhamana na shauri limepangwa kutajwa tena Novemba 13, 2023 kwa kuwa uchunguzi bado  haujakamilika

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI