IKIWA ni siku mbili toka katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Taifa Paul Makonda kutoa agizo la miezi sita kwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa kutatua kero ya ardhi nchini , mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kanda ya Nyasa mchungaji Peter Msigwa amesema agizo hilo ni kinyume na katiba ya nchi kwani waziri mkuu anagizwa na Rais sio wasemaji wa vyama.
Akizungumza na Matukio Daima Media leo mjini Iringa kuhusu maoni yake juu ya agizo la Makonda kwa waziri mkuu na mawaziri nchini ,mchungaji Msigwa alisema kuwa amesikitishwa na jinsi ambavyo katiba ya nchi inavyovurugwa na msemaji wa CCM kwani kazi ya msemaji si kumuagiza waziri mkuu ama waziri yeyote ndani ya nchi kwani mawaziri wapo kikatiba na katiba na nchi inaongozwa na katiba ya nchi sio katiba za vyama .
“ Nasikititika sana kuona watanzania waliwengi hawapendi kusoma katiba yetu na ndio maana kwa sasa baadhi ya watu wanashangilia matamko ya Makonda kwa waziri mkuu na mawaziri anafanya haya kinyume kabisa na katiba ya nchi yetu kewani waziri mkuu na baraza la mawaziri limetajwa kwenye katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania waziri mkuu ni kiongozi wa heshima kama kuna matatizo yao ndani ya CCM waongee ndani ya vikao vyao sio nje ya chama “ alisema Mchungaji Msigwa .
Alisema kuwa kwenye katiba ya nchi hakuna sehemu ambayo imetaja Mwenezi wa chama chochote cha siasa hivyo ni wazi waziri mkuu ama mtumishi yeyote wa serikali anapaswa kuheshimiwa bila kujali anatokana na chama gani cha siasa .
Hata hivyo mchungaji Msigwa alisema mbali ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kutowatambua wenezi wa vyama vya siasa ila hata katiba yao CCM hakuna sehemu ambayo inampa nguvu Mwenezi wa chama kumuagiza waziri mkuu ama waziri yeyote zaidi ya kukisemea chama chake .
Alisema ndani ya katiba yao CCM kazi ya idara ya itikadi na uenezi imeeleza wazi majukumu yake ambayo ni kueneza na kufafanua itikadi na sera za CCM , kupanga na kusimamia mafunzo na maandalizi ya makada na wanachama ,kusimamia vyombo vya habari vya chama ,mawasiliano na uhamasishaji wa umma kwa ujumla ,kuongoza na kusimamia maandalizi ya Programu na ilani za uchaguzi za CCM , Kusimamia utafiti ,maktaba na nyaraka za CCM pamoja na kushughulikia masuala ya msingi ya itikadi na sera za CCM na si vinginevyo .
“ Hii ndio kazi ya Mwenezi sio kutoa matamko hana mamlaka hiyo nadhani alikuwa anapiga porojo na kwa kuwa watu wengine hata wana CCM wengi hawajui anamuita mkuu wa mkoa pale kama mtoto ana muita waziri kama mtoto hii ni kinyume na tusitengeneze utamaduni kama huu mtu ambae hana mamlaka kutoa kauli kama hizi “alisema Mchungaji Msigwa
Kuwa hana ugomvi wowote na Makonda ila hakubaliani ni njinsi ambavyo Makonda anavyotaka kuvuruga katiba ya nchi na kujipa madaraka makubwa ambayo katiba haimtambui kwani mwenye mamlaka ya kumuagiza waziri mkuu ama waziri yeyote ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na sio vinginevyo.
Pia alisema anashangazwa na tabia iliyozuka ndani ya CCM ya viongozi wa chama kufanya ziara ya kukagua miradi wakati wanao wawakilishi wa wananchi kwa maana ya Rais ,mbunge na diwani ambao ndio wanapaswa kusimamia miradi na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo kwenye vikao vya ndani vya chama ambako huku wanaweza kuwahoji hata mawaziri ila sio kutoka hadharani hivi .
Hata hivyo alisema kinachoendelea ndani ya CCM kwa sasa ni kama wajenzi wa mnala wa Babeli jambo mbalo kwao upinzani wanaanza kuona wazi ni namna gani ambavyo CCM inakwenda kuachia madarakana kwani japo wao wanafurahia ugomvi wao wa ndani kuja hadharani kama hivi kwa kuonza kuonya wastaafu wao.
0 Comments