Header Ads Widget

JESHI LA POLISI IRINGA NA OPARESHENI MAJANGILI, HUKU MFUNGWA ALIYETOROKA AKAMATWA TENA

 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa Alan Bukumbi Leo 21/11/2022 akizungumza na vyombo vya Habari amesema, Kwa ujumla hali ya Mkoa wa Iringa ni shwari, Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa katika kuimarisha ulinzi na usalama linaendelea kufanya doria na misako mbalimbali ilikubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu ambapo limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa pamoja na vitu mbalimbali.

Katika operesheni na misako iliyofanyika kuanzia Novemba 11, 2023 hadi Novemba 20, mwaka huu, kwa kushirikiana na Askari wa uhifadhi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama tumefanikiwa kukamata jumla ya watuhumiwa thelathini na nne (34) kwa makosa mbalimbli kama vile kupatikana na silaha kinyume cha sheria, kupatikana na nyara za serikali, kuingia hifadhini bila kibali, kupatikana na sumu na kujihusisha na ujangili.

Aidha katika Operesheni hiyo silaha kumi na moja (11) zimekamatwa, silaha aina ya Gobore 10 na silaha aina ya shortgun moja pamoja na Goroli sabini na saba (77), baruti kiasi cha robo lita, silaha sita kati ya hizo zilitelekezwa na wamiliki ambapo Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama linaendelea kufanya uchunguzi kuwabaini wamiliki wa silaha hizo, silaha hizi zimekuwa zikitumika katika uwindaji haranu na ujangili pamoja na matukio mengine ya kihalifu.

Vitu vingine vilivyokamatwa ni pikipiki mbili MC.326 CJK aina ya HAUJUE rangi nyekundu na Pikipiki aina ya Fekoni chesisi namba LDAPAJOB8LGB02359 ambayo haina namba za usajili zilizotumika katika kusafirisha nyara za serikali pamoja na vifaa kama shoka moja kisu kimoja, vipande vitano vya nondo,msumeno mmoja, mikuki sita, mapanga mawili, unga wa baruti, nyaya ishirini na saba (27). Watuhumiwa wote waliolamatwa watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Vilevile novemba 17,2023, majira ya saa 02:00hrs huko maeneo ya kijiji cha Nyang'oro kata ya nyang'oro tumefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja aitwaye James Mtewele (40) mkulima na mkazi wa kijiji cha Migoli akiwa amebeba madawa ya kulevya aina ya bhangi ikiwa imehifadhiwa katika gunia moja la kilo mia moja akisafirisha kutoka maeneo ya llula kwenda kijiji cha Migoli. Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Halikadhalika tumemefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja aitwaye Edger Mbalanzi ambaye alitoroka mahakamani, aliyekuwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 22/2018 kosa kupatikana na nyara za serikali Meno ya Tembo ambaye atatumikia kifungo chake cha miaka Ishirini jela.

Katika hatua nyingine Kamishna Msaidizi Mwandamizi na Kamanda wa Hifadhi ya Taifa Ruaha, Godwell Ole Meing’ataki, alifafanua namna vijana wengi wanavyotumika katika biashara haramu hususani ujangiri. Pia alieleza namna risasi za kisasa na za kienyeji zinavyotumika kuulia Wanyama, walizokamatwa nazo watuhumiwa huku zingine zikitengenezwa na watu wanaotengeneza silaha haramu kama vile bunduki aina ya short gun na Gobole ambazo nazo pia zilikamatwa katika oparesheni hiyo .

‘’..Majangiri wamekuwa hawachagui silaha, Kama ambavyo tunaona kuna sime, panga, mundu, Nyaya na silaha nyinine nyingi za jadi ambazo hutumika katika shughuri zao hasa majira ya usiku ambapo hutumia tochi zenye mwanga mkali na hata mbwa pia.  Lakini pia sumu inayotumika kuulia Wanyama mbalimbali ambapo hasa katika kipindi ambacho mtu Ruaha umekauka, majangiri huingia na kumwaga sumu hizo kwenye madimbwi mbalimbali na kuua Wanyama wadogo kwa wakubwa, na isivyo bahati  nyama hizo huuzwa kwa watu, hivyo wananchi wanaopenda kula nyama za wanyamapori wanaombwa kuacha kwani ni hatari kwa afya zao..’’

Kamanda Uhifadhi aliongeza juu viungo vya wanyama waliokutwa navyo majangiri katika oparesheni hiyo ni Pamoja na kucha za Mhanga, Ngozi ya Sungura, Meno ya Tembo, Pamoja na Kakakuona ambao soko lao has ani soko la nje ambako huko hununuliwa kwa matumizi mbali mbali, huku wakiacha athari kubwa katika maeneo ya uhifadhi nchini.

Jeshi la Polisi mkoa wa Iringa linatoa wito kwa wananchi kuendelea kushrikiana na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu, na wote wanaojihusisha na matukio hayo waache mara moja kwani jeshi la polisi pamoja na askari wa wanyama pori wamejipanga kuhakikisha uharifu wa aina zote unatokomezwa.

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI