Header Ads Widget

WANUSURIKA KIFO KWA TUHUMA ZA UCHAWI

Salum Kali Mkuu wa wilaya Kigoma

Salum Kali Mkuu wa wilaya Kigoma na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wakifanya ukaguzi eneo lilipotokea tukio
Gaston Kabage mkazi wa kijiji cha Mushenyi Kigoma Vijijini  ambaye alinusurika kuuawa  kwenye tukio la nyumba yake kushambuliwa kwa tuhuma za uchawi
 

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

Watu wawili wakazi wa kitongoji cha  Mushenyi  kata ya kalinzi wilaya ya kigoma wamenusurika kifo baada ya kujeruhiwa, kuporwa na  kuharibiwa  kwa  mali zao  kulikofanywa na baadhi wananchi wa kijiji hicho wakiwawatuhumu  kujihusisha na vitendo vya imani za kishirikina.


Mmoja wa waathirika wa tukio hilo, Gaston Kabage akieleza tukio hilo  mbele ya kamati ya ulinzi na usalama   ya wilaya ya kigoma amesema kuwa   vitendo alivyofanyiwa si vya kiungwana na wanakijiji wenzao  kwa madai  ya kuwabaini kuwa wao ni wachawi kupitia upigaji wa ramli.


Alisema kuwa alinusurika kuuawa baada ya kutoroka kupitia mlango wa nyuma kufuatiwa wanakijiji wenzake kuvunja mlango wa mbele wakitangaza kumsaka huku wakiwa na mapanga na Marungu.


Kwa upande wake mtoto wa mwenye nyumba hiyo,Dainesi Gaston alisema aliona kundi kubwa la watu linavamia  nyumba yao kwa kurusha mawe juu ya bati, kuvunja vioo vya madirisha na kukatakata migomba hivyo alipiga kelele kumwita baba yake ili ashuhudie hali hiyo.


Akizungumza kwa nyakati tofauti Mkuu wa wilaya  ya Kigoma,  Salumu Kali ambaye  pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya hiyo amekemea vitendo hivyo na kutangaza  kuwa serikali itachukua hatua madhubuti kwa wale wote waliohusika na kushiriki kwenye vitendo hivyo.


Kali alisema kuwa kupitia kamati ya ulinzi ya wilaya wameanza kubaini waliotajwa kuhusika na vurugu hizo na kwamba watatembea nyumba lwa nyumba kuwakamata wahusika.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI