Header Ads Widget

WANAODAI FEDHA ZA MALIPO YA TUMBAKU WATALIPWA MWEZI HUU.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewahakikishia wakulima wa  zao la Tumbaku   katika msimu wa kilimo 2022/2023 ambao  hawaja lipwa   fedha zao zaidi ya Dola Milioni 2.5 kwenye Amcos 6 zilizoingia Mkataba wa ununuzi wa Tumbaku na Kampuni ya Mkwawa Leaf LTD  zinatarajiwa kulipwa hivi karibuni na  kampuni hiyo. 


Kwa  mujibu wa taarifa  iliyotolewa kwa vyombo vya  habari RC Mrindoko  amesema  anawahakikishia  wakulima   wa Amcos  sita  ambazo  hazijalipwa  Fedha ya mauzo  ya Tumbaku  tayari serikali imefanya jitihada Kupitia   Rais  Dkt  Samia   Saluhu  Hassan amefanya  jitihada kubwa  za kuhakikisha wakulima hao wanalipwa  fedha zao  hivi karibuni  kuanzia tarehe 1 oktoba na kuendelea wataanza kulipwa .


Amebainisha kuwa Serikali ya Mkoa wa Katavi  inafahamu  kuna  wakulima  wa Tumbaku  hawajalipwa   fedha zao kwa wakati walizouza  Tumbaku yao  kwa  msimu   wa mauzo ya tumbaku ya  mwaka huu.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI