Header Ads Widget

ISRAEL: WANAFUNZI WAWILI WA KITANZANIA BADO HAWAJAPATIKANA

 


Balozi wa Tanzania nchini Israel, Alex Kallua amesema bado hawajapata taarifa upatikanaji wa wanafunzi wawili kutoka Tanzania ambao wapo nchini Israel kwa masomo, baada ya kupoteza mawasiliano nao toka nchi hiyo iliposhambuliwa na kundi la Hamas mwishoni mwa wiki iliyopita.

 

Akizungumza katika mahojiano na BBC amesema “sisi kama ubalozi tumetumia kila namna tunavyoweza kutafuta ukweli wa hawa ndugu zetu, wako wapi au nini kimetokea, hivyo tutakapopata taarifa sahihi tutazitoa.”

 

Balozi Kallua aliiambia BBC kuwa wanaendelea kufuatilia hali ilivyo katika maeneo mbali mbali na kuhakikisha watanzania wote wapo salama ikiwemo kubaini walipo raia hao wawili.

 

“Hatuwezi kutoa taarifa za kukisia kwani tunaendelea kufuatilia kwa mamlaka za Israel ili kupata taarifa sahihi… sisi tupo hapa ‘on the ground’ tunafuatilia watanzania wote waliopo hapa, kuhakikisha usalama wao.” alieleza.

 

Chanzo: BBC Swahili


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI