Header Ads Widget

RPC BUKUMBI AWATAKA WAZAZI KUWA MAKINI MALEZI NA ULINZI YA WATOTO WAO

 


Na Mwandishi wetu Iringa

Ili mtoto kike ajisikie kuwa anaishi katika dunia sawa ana hii wanayoishi watu wengine, wazazi/walezi wanatukiwa watimize majukumu yao kwa kuhakikisha usalama wa mwanae.


Hayo yameelezwa na Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Allan Bukumbi (Kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa), akiongea na vyombo vya Habari makao makuu ya jeshi la polisi mkoa wa Iringa, amesema kesho tar. 11/10 kutakuwa na kilele cha maadhimisho ya mtoto wa kike duniani, , yenye kauli mbiu "wekeza katika haki za wasichana, uongozi wetu, ustawi wetu".


“Kiujumla yanaandaliwa kupitia dawati la Jinsia na Watoto la jeshi la polisi, lakini huu ni mpangokazi unaotolewa na umoja wa mataifa kuhusu usawa wa kijinsia na haki za mtoto wa kike duniani” amesema kamanda Bukumbi.


Pia Kamanda Bukumbi amesema kuwa, hii ni fursa kwa wadau mbali mbali kuelewa jukumu lao kuhusu mtoto wa kike, na kimsingi changamoto zinazowakabiri Watoto wa kike. Kuna wadau mbalimbali kama wazazi/walezi wajue wajibu wao ni nini kwahiyo watapata elimu.


"Sisi kama jeshi la polisi tunajukumu la kusimamia sheria ambayo inamuhusu mtoto wa kike, na kuzuia kadhia inayompata mtoto wa kike kama vile mimba za utotoni, mila gandamizi, kubaguliwa na matukio mengine jinai wanayofanyiwa katika maeneo mbalimbali wanayoishi".


Aidha kamanda amebainisha kuwa serikali inajukumu kubwa pia kupitia taasisi mbalimbali tofauti na jeshi la polisi wapo Ustawi wa Jamii, zipo mahakama na idara nyingine zinazoshughulikia masuala ya mtoto wa kike.


Kamanda anawakaribisha wananchi wote ikiwemo taasisi mbalimbali za serikali, mashirika ya umma na binafsi, shule na vyuo kushiriki maadhimisho hayo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI