Header Ads Widget

KIJANA WA KITANZANIA ABUNI TEKNOLOGIA YA KUZUIA AJALI YA TRENI NA VYOMBO VYA MOTO UKIWEMO MAGARI

 

Alvine Antony; Muhitimu wa  chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), aliyebuni  teknolojia  itakayozuia ajali  kati  ya treni na vyombo vya moto.

Hii ndio teknolojia bunifu itakayozuia ajali kati ya treni na vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki ambazo zimekuwa zikitokea katika makutano ya njia za reli na barabara.


Na Lucas Raphael,Tabora

 

Muhitimu wa  chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)  Alvine Antony  amebuni  teknologia  itakayozuia ajali  kati  ya treni na vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki ambazo zimekuwa zikitokea katika makutano ya  njia za reli  na barabara.

 

Akizungumza na waandishi wa habari jana wakati akielezea  mfumo huo katika maonesho ya  maadhimisho ya  usalama wa reli ambayo yanafanyika  kitaifa mkoani Tabora .

 

Alisema kwamba mfumo huo  ameuunda ukiwa na uwezo wa kutambua ikiwa treni inapokaribia makutano ya  barabara  na reli taa za barabarani ziwake kuzuia magari, na mageti yanafunga pande zote  na kuruhusu treni kupita na badaye milango  hiyo  kufunguka ili kuruhusu vyombo vya moto kupita na watembea kwa miguu baada ya treni kupita eneo la makutano. 

  

Alvine alisema kwamba amefanya ubunifu huo kwa muda wa mwezi  mmoja wakati wa masomo yake katika chuo hicho.

 

Hata hivyo aliiomba serikali na wadau wa usafiri wa reli kumshika mkono katika  kuboresha bunifu hiyo ili kupunguza ajali katika makutano ya reli na barabara.

 

Aidha alisema kuwa  teknolojia hiyo inaweza kutumika  katika  kusaidia kuondokana na wimbi la ajali ambazo zimekuwa zikitokea katika  makutano ya njia za reli na barabara nchini

 

Juma Manday; Afisa uhusiano wa NIT akisisitiza jambo juu ya teknolojia ambaye anasema itakuwa mwarubani wa kwa kuzuia ajli kwenye makutano ya barabara na reli.

Afisa uhusiano wa NIT Juma Manday alisema kwamba teknolojia hiyo ndio itakuwa mwarubaini wa kupunguza kutokea kwa ajali kwenye makutano hayo.

 

Alisema maeneo hayo yanakubwa na matukio ya ajali za mara kwa mara lakini uwepo wa teknolojia hiyo kutoka katika chuo cha Taifa cha Usafirishaji itasaidia kwa asilimia kubwa kupunguza ajali hizo.

 

Alitoa wito kwa wadau mbalimbali watembelee banda la chuo cha Taifa cha usafirishaji ili kupata maelezo ya kozi mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho.


mwisho

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI