Header Ads Widget

WAPELEKENI WATOTO WAPATE CHANJO YA POLIO

Na Elizabeth Ntambala Rukwa

Mganga mkuu wa mkoa Ibrahim Isaack  amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la utoaji wa chanjo kwa watoto chini ya miaka 8 ili kujikinga dhidi ya ugonjwa wa Polio.


Kauli hiyo imetolewa leo  wakati wa uzinduzi wa kikao cha Waandishi wa habari juu namna ya kujikinga pamoja na kutoa elimu kwa wananchi  juu ya ugonjwa wa polio


Aidha Mganga mkuu lsack  amesema kuwa kila mtoto wa mkoani Rukwa anapaswa kupata chanjo ya polio kwani itaongeza kinga mwilini na kumuepushia mtoto ulemavu wa kudumu au hata kifo kwani ugonjwa huo hauna tiba.

 Amesisitiza kuwa wazazi  wanatakiwa kuto waficha watoto ndani  ili  waweze kupata  haki zao za kuwa na afya njema na kuacha mila potofu kwani kufanya hivyo kutaleta madhara makubwa katika jamii.


Kwa upande wake Mratibu wa chanjo mkoa Ndenisia Ulomi  amebainisha kuwa malengo ya Mkoa wa Rukwa ni kuwafikia watoto 391,883 kwa kuwapatia chanjo aina ya pili ya polio katika vituo vya Afya na nyumba kwa nyumba. Ndenisia amewataka wananchi kutoa taarifa za viashiria vya ugonjwa wa polio katika kituo cha afya iwapo dalili za mtu mwenye viashiria vya polio ikionekana ili iwe rahisi kuudhibiti.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI