Header Ads Widget

TUNDU LISSU NA WENZAKE WASHIKILIWA NA POLISI



Na Simon Joshua - Matukio Daima App, Arusha.

Makamu Mwenyekiti wa chama Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania,CHADEMA na mgombea urais kupitia chama hicho katika Uchaguzi mkuu wa 2020, Tundu Lissu anashikiliwa na Jeshi la Polisi.


Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha, Lissu amekamatwa leo Karatu Arusha, alikokuwa anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Mazingira Bora.


Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Lissu, mbunge wa zamani na mwanasheria, ambaye aliwahi kunusurika kuuawa kwa kupigwa risasi 16 miaka 6 iliyopita anatuhumiwa kwa makosa mawili; kufanya mikusanyiko bila kuwa na vibali na kuzuia Polisi kufanya kazi yao.

Taarifa ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Justine Masejo inaeleza Lissu na viongozi wengine watatu wa chama hicho, watahojiwa na Polisi na utaratibu mwingine wa kisheria kuendelea.


Kwa mujibu wa viongozi wa CHADEMA, kabla ya kumamatwa kwa Lissu, hoteli aliyofikiwa kiongozi huyo inayoitwa Ngorongoro na nyingine ya Panorama huko Karatu zilizingirwa na Polisi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI