Header Ads Widget

RPC LINDI - ALIEJIKATA UUME NI MGONJWA WA AKILI

 


NA HADIJA OMARY,LINDI 

Jeshi la polisi mkoani Lindi limethibitisha kuwa kijana simoni manyoli (30) mkazi wa mtaa wa msonobalini chini kata ya msinjahili Manispaa ya Lindi Mkoani humo aliejikata sehemu yake ya siri (uume) yeye mwenyewe ni mgonjwa wa akili

 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa Habari na kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi ACP Pilli Omary Mande  alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa tatu kamili asubuhi ambapo kijana huyo alijikata kwa kutumia kitu chenye ncha kali sehemu za siri (uume na kuundoa akabisa) akiwa chumbani kwake kwenye nyumba aliyopanga.

 



ACP pilli Mande alisema Mtu huyo mara baada ya kujikata alitoka katika chumba chake akiwa uchi na damu zikimtoka nyingi huku akikimbilia baharini ambapo alipofika alianza kuosha jeraha hilo kwa maji ya bahari.Hata hivyo raia wema walitoa taarifa kituo cha Polisi na hatimaye Polisi walifika na kumchukuwa kisha walimpeleka kupatiwa matibabu katika hospitali ya Sokoine Lindi.

 


Aidha alibainisha kuwa Muhanga huyo alikuwa ni muajiriwa wa kampuni ya Moset Traders iliyoko wilaya ya Lindi ambaye meneja wake Hegera Werema,24 amesema Muhanga alifika ofisini akiwa na msongo wa mawazo na ndipo alimuuliza anamatatizo gani lakini alidai hayupo sawa ndipo alimpatia ruhusa aende akapunzike ndipo baada ya muda tu kumruhusu alipata taarifa za kujikata sehemu zake za siri.

 

Alisema Jeshi la Polisi liliweza kubaini ndani ya chumba chake ambacho anaishi peke yake, chupa ndogo ya kilevi aina ya Smart Gin ambayo ilikuwa nusu pamoja na dawa ambazo madaktari walisema zilikuwa ni za kutibu magonjwa ya zinaa.


 

Hata hiyo kwa mujibu wa kamanda wa polisi alisema  meneja huyo amebainisha kuwa Muhanga anahistoria ya kuugua ugonjwa wa afya ya akili kwa muda wa mwaka mmoja kipindi cha nyuma ,na alilazwa katika wodi ya watu wenye matatizo hayo katika hospitali ya Bugando mkoani Mwanza.Ameongeza kuwa amekuwa na tabia ya kuvua nguo hali hiyo inapomrudia na hasa anapokuwa na msongo wa mawazo.Muhanga amelezwa katika hospital ya Sokoine akiendelea kupatiwa matibabu.

 

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI