NA MWANDISHI WETU, MTWARA
Wakulima wa zao la muhogo Wilaya ya Mtwara wamefurahia ufundishwaji wa teknolojia katika mashamba darasa ya zao la muhogo yaliyowekwa katika Kata mbalimbali Wilayani humo.
Akizungumza wakati wa kuvuna mihogo katika shamba darasa la Kata ya Mkunwa Mtafiti wa mazao jamii ya mizizi ya viazi na mihogo kutoka taasisi ya utafiti wa klimo Tanzania TARI kituo cha Naliendele Festo Masisila alisema kuwa wanazo aina mbalimbali za Tricas 1,2,3,4 na 5 ambazo zimedhibitishwa na Taasisi ya Tosc mwaka 2009.
Alisema kuwa kupitia mashamba darasa wakulima wamejifunza kuanzia kuandaa mashamba mpaka uvunaji na namna ya kuyabaini magonjwa batobato kali pamoja na michilizi kahawia.
"Tuliweka shamba darasa ili wakulima waweze kuwa na machaguo kulikngana na sifa mbalimbali za mbegu ambapo mbali na Taricas pia zipo mkumba, chereko, mkuranga, kiroba na kipusa mkulima anachagua mbegu gani inafaa Kwa biashara na chakula" alisema Masisila
Nae Mussa Liponda afisa kilimo kata ya Mkunwa alisema kuwa TARI wamefanya jambo kubwa Kwakuamua kutuletea mashamba darasa ya mihogo.
"Wakulima wengi wameshangaa tulipanda miezi michache sana na tumepatapata mavuno mengi mbegu hizi zinafaa Kwa Kilimo biashara sasa tunaweza kuhama kutoka kwenye mbegu za asilia na kuanza kulima mbegu bora kwakutazama muhogo kibishara na kwa mihogo mibichi
Nae Fatuma Rambaramba mkulima wa muhogo Kata ya Mkunwa alisema kuwa mbegu hizo zinafaa Kwa Kilimo biashara.
"Mfano mbegu ya kiroba nimeiona ni mbegu bora ukipanda mapema unavuna mapema na inajaa sana kwenye shina hivyo inakuwa mihogo mkubwa zaidi haina madoa haishambuliwi na magonjwa kama mihogo mingine" alisema Rambaramba
0 Comments