Header Ads Widget

MADEREVA WA MALORI NA MABASI 200 WARUDIA DARASANI VETA IRINGA


ZAIDI ya madereva  malori na mabasi  200 katika mkoa wa Iringa  wamerejeshwa  darasani  kunolewa  zaidi  juu ya  sheria  za  usalama  barabarani  kama  mkakati  moja wapo  wa  kupunguza ajali za  barabarani  zinazosababishwa na baadhi ya madereva  waio na  weledi  wa kazi  hiyo .

Akifungua jana mafunzo hayo ya  udereva ya  wiki mbili yaliyoandaliwa na  chuo  cha Ufundi  stadi  VETA  mkoa  wa  Iringa  kamanda  wa  polisi wa  mkoa wa Iringa Allan Bukumbi   alisema  kuwa  Taifa   linashtushwa  sana na matukio ya  ajali  za barabarani  zinazotokea hususani  za mabasi ,malori na magari  mengine  yanayobeba  abiria  hivyo  kupitia  mkakati  huo  wa  kuwarudisha  darasani] madereva  utasaidia  kupunguza  ajali  .


 Alisema  kuwa ajali  nyingi  zinasababishwa na  uzembe  wa madereva  na kuwa pamoja  na juhudi kubwa  za jeshi la polisi  na wasimamizi wengine wa sheria  kuendelea  kutoa  elimu ,kuonya na kufanya oparesheni  mbali mbali  bado  jeshi la polisi mkoa wa Iringa  litaendelea  kuchukua hatua  kali na madhubuti  za  kukabiliana na hali  hiyo ya ajali .


Bukumbi  alisema  ajali nyingi  zimekuwa zikicvhangiwa na sababu mbali mbali  kama  maddereva  wa magari  na  pikipiki  kuwa sehemu  kubwa ya  vyanzo  vya  ajali kwa  kutiozingatia   sheria  kwa  kuendesha  kwa  mwendo kasi bila kujali  ukomo  wa mwendo  elekezi  wa  kisheria  ,kuyapita magari  ya mbele yao  bila kuchukua tahadhari,kuendesha magari mabovu barabarani  pamoja na kuendesha  vyombo hivyo vya moto  bila kupata mafunzo katika  vyuo vya udereva na baadhi  yao kutokuwa na leseni  za  udereva .


Hata  hivyo  alisema  kuwa   kupitia  mpango  huo  wa  serikali kutaka  madereva  wote  kurudi  vyuo ili  kupata mafunzo ya  udereva ni  wazi  utasaidia  sana   kupunguza ajali kwa kuwa na madereva  wenye  sifa  za  vyuoni  vya udereva .


" Chuo  hiki  cha  VETA  kina  wakufunzi mahiri  ambao  tunaamini  kwamba  watawapika  vizuri  na  mtaiva   vizuri  kwa  wale  ambao mtazingatia  masomo  yote  ya  darasani na  vitendo "  alisema  Bukumbi 




Mratibu  wa mafunzo hayo  Edmund Enugu  alisema  kuwa  jumla ya  madereva  200  wa malori na mabasi ya abiria   wameanza mafunzo hayo ya  wiki  mbili na kuwa baada ya mafunzo hayo  watapanda madaraja  ya  awali   na kufikia madaraja  ya juu  ya  kuendesha  magari ya abiria na mizigo (PSV na   HGV) . 


Kwa upande  wake  mkurugenzi wa  VETA kanda  ya  nyanda  za  juu kusini  Suzana Magani  alisema  kuwa  chuo  hicho  kimeendelea  kutoa  mafunzo  ya  udereva  na mafunzo  mengine  na  kutoa  wito  kwa  wale  wanaohitaji  kupatiwa mafunzo mbali mbali  kuendelea  kujiunga na  vyuo  vya  VETA  ili kupata ujuzi  kamili .






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI