Header Ads Widget

BABA AJIFUNGIA NDANI NA WATOTO WATATU AJIUA KWA MOTO

 



Mwanaume  mmoja mkazi  wa  kitongoji  cha Darajani kijiji  cha Malolo   wilaya ya  Kilosa mkoani Morogoro alitajwa  kwa  jina la Aman Malekela (72)  amejiua kwa  kujichoma  moto ndani ya  chumba chake  yeye na  watoto  wake  watatu kwa  kile  kinachodaiwa ni  msongo  wa mawazo  kutokana na maradhi  yaliyokuwa  yakimsibu  pamoja na ugumu  wa maisha .


Wakizungumza Leo  na mwandishi wa Matukio Daima Media   aliyefika  eneo la  majirani wa  marehemu  huyo  walisema  kuwa  siku  zote  enzi za uhai  wake marehemu  alikuwa akilalamika  hali  duni ya maisha  kiasi cha  kushindwa  kupata   fedha  ya matibabu ya  ugonjwa  uliokuwa  ukimsumbua.


Alisema mmoja kati ya majirani wa  marehemu  huyo Aman Alli  kuwa  siku  moja kabla ya kifo chake  walikutana  na kubwa  alikuwa  akilalamika kukosa   fedha  za mahitaji ya  nyumbani pamoja na fedha  za matibabu za  ugonjwa  ambao  alidai  ulikuwa  ukimsumbua  (bila  kutaja ugonjwa  huo)  alisema ni muda  mrefu amekuwa  akiumwa na akijiuguza  mwenyewe .


Hata  hivyo  alisema  taarifa  ya tukio la  kifo  cha mzee  huyo na watoto wake  alikipata kwa  majirani na  baada ya  kufika  katika nyumba  yake  walishuhudia  moto  mkubwa  ukiendelea kuwaka ndani ya  chumba  chao  kabla ya  wananchi  kuchukua hatua  ya  kuzima  moto  huo ambao  hata  hivyo tayari   uklikuwa  umekwisha  sababisha   vifo  vya  mzee  huyo na watoto  wake  watatu .



Angela Malekela Madunda  ni mjukuu  wa mzee  huyo  ambae ni mhanga  wa  tukio  hilo  alisema  kuwa  juzi  majira ya saa 3 usiku  baada ya  kurejea  nyumbani hapo  alikuta mzee  wake  huyo akiwa ametoa chumbani  kwake  sebuleni  cherehani na vitu  vingine  vya  thamani   na  baada ya  kumuuliza  sababu ya  kuvitoa  vitu  hivyo  ndani alimjibu kuwa amefanya  hivyo kwa  usalama  wa  vitu  hivyo .


" Sikujua kama  babu anataka   kufanya maamuzi mazito ya  kujiua na  watoto  wake ndani  maana  baada ya  kutoa  vitu  hivyo aliwaita  watoto hao  watatu na  kuingia nao ndani  kulala  kitanda  kimoja na  usiku  muda kama wa saa 7 usiku  hivi  mimi  nikiwa  nimelala  chumba  cha  pili   nilishtushwa na  joto kali  ndani ya  nyumba  pamoja na moshi  mzito uliokuwa  ukitoka  chumbani kwa  babu"  alisema   binti  huyo mwenye  miaka kati ya 27 .


Kuwa yeye  alikuwa amelala na mtoto wake  chumbani na  baada ya  kuona  hali  hiyo ya moto  alitoka  nje na mtoto  na kuanza kupiga kelelea  kuomba msaada  kwa majirani ambao  walifika na kuanza kuzima  moto  huo .


Alisema  kwa kawaida  watoto hao  watatu  huwa  wanalala  kwa zamu  kwa mama  yao  aliyepo  ng'ambo ya  pili ya daraja  kwa maana ya  wilaya ya  Kilolo  mkoa  wa Iringa  na baba yao  ambae  yupo  upande wa Kilosa na  siku  hiyo ya  tukio  walikuja  kulala kwa  baba yao kama  kawaida .


Kuwa mzee  huyo  alitengana na mke  wake na  hivyo  siku  zote  amekuwa akiishi  mwenyewe na  yeye kama  mjukuu na  watoto  hao ambao  wamekuwa  wakija kwa  zamu  kulala  na baba  yao.


Hata   hivyo  alisema   nyumba   hiyo  haikuwa na umeme wala  ndani  hakukuwa na kibatali ,taa  wala aina  yoyote ya  moto  na anashangazwa na  chanzo  cha  moto  huo  usiojulikana  ambao  wamepelekea  vifo  vya  ndugu  zake ni  wapi umetokea.


Mwenyekiti  wa  serikali ya  kijiji  hicho Sufian  Ramadhan  alisema  kuwa  wao kama  serikali ya  kijiji  baada ya  kupata  taarifa ya  moto  huo walikimbia  kituo  cha Polisi  Ruaha  Mbuyuni kutoa  taarifa  na  polisi  walipofika  walikuta  tayari vifo  hivyo  vimetokea .




Kamanda  wa  polisi  wa  mkoa  wa  Morogoro Alex Mkama alithibitisha  kutokea kwa  tukio  hilo  na kuwataka  wananchi kuendelea  kuwa  watulivu  wakati  jeshi la  polisi  linaendelea na uchunguzi  wa  tukio  hilo .


Kamanda Mkama  alisema uchunguzi  wa awali  unaonesha   chanzo  cha vifo   hivyo  ni  moto  ambao  uliwashwa   ndani ya  chumba  hicho  baada ya maandalizi yote ya  moto  huo  kufanywa na mzee  huyo .


Kwani alisema  wamebaini  kuwa  kabla ya  kujiteketeza kwa  moto  marehemu na  watoto  wake  walijifungia ndani ya  chumba  hicho na  kuwa  marehemu  alikuwa  mnufaika wa  mradi wa TASAF .


Aliwataja  waliofariki  dunia kwa  moto  huo kuwa ni Aman Malekela Madumba (72) ambae ni baba  wa  watoto hao pamoja na watoto  wake  Habibu  Madumba (10), Sadiki Madumba (8) na Bahath Madumba (5) ambao wote  walikuwa ni   wanafunzi wa  shule ya  msingi .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI