JESHI
la polisi mkoa wa
Iringa linamshikilia Amani
Martin maarufu kwa jina la Kasisi
(47) mkazi wa Nzihi
wilaya ya Iringa ambae pia ni kiongozi wa dini kwa tuhuma
za kumlawiti mtoto
wake mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi
saba kwa madai ya kudanganywa na shetani.
Kamanda wa
polisi wa mkoa wa Iringa Allan
Bukumbi aliwaeleza wanahabari leo ofisini
kwake kuwa tukio hilo lilitokea Machi 28 majira ya saa saba mchana na
kumsababishia maumivu makali
sehemu za haja kubwa .
Alisema kuwa Kasisi ambae ni mkulima wa Kijiji
cha Nzihi alidai kuwa alifanya tukio hilo baada ya
kudanganywa na shetani na kuwa anajutia
kutenda unyama huo kwa mwanae .
Alisema kuwa mama wa
mtoto huyo Magreth Kaguo (29) ndie
ambae alibaini mtoto
wake huyo kulawitiwa na
kuwa mtuhumiwa amekamatwa na
atafikishwa mahakamani wakati wowote .
Katika tukio
jingine jeshi la polisi
linamshikilia mtuhumiwa mmoja jina limehifadhiwa kutokana na sababu za kiuchunguzi ambae anatuhumiwa
kukodisha silaha kwa wahalifu .
Kamanda
Bukumbi alisema kuwa mtuhumiwa
huyo mkazi wa eneo la Kihesa Kilimani Manispaa ya Iringa
alikamatwa April 3 majira ya 11 jioni baada ya taarifa
fichi kutoka kwa wasamaria
wema kuhusiana na biashara isiyo rasmi ya ukodishaji silaha mbili aina ya
shotgun yenye namba za usajili TZ
CAR 6271 na Rifle yenye namba za usajili CAR 48081 ambayo imepelekwa kikosi cha mizinga mkoa wa Morogoro kwa ajili ya matengenezo ,kuwa kupitia mwanya huo amekua akijipatia fedha
kwa njia ya kukodisha silaha na
risasi kwa kiasi cha shilingi 100,000 kwa tukio .
“
mtuhumiwa huyo amekuwa akikodisha silaha
hizo kwa watu mbali mbali kitu ambacho
ni kinyume na utaratibu wa matumizi ya silaha na sheria
za nchi .
Kamanda Bukumbi alisema tukio
jingine ni lile lililotokea April 4 mwaka huu eneo la Mwangata A kata ya Mwangata Manispaa ya Iringa kwa
jeshi hilo kufanya msako na kufanikiwa kukamata silaha
aina ya Pistol Rami yenye namba za usajili A935520 pamoja na risasi zake 10 ndani ya Magazine ambayo ilisalimishwa karibu na nyumba ya mwenyekiti wa mtaa wa Mwangata A Batista Kisonga baada ya mtuhumiwa Rashid Nyomolelo kuiba kutoka kwa Joseph Philipo Lukonde (44) mkazi wa Nkuhungu mkoani Dodoma
mtuhumiwa bado anatafutwa .
Wakati huo
huo Julius Mlwale(36) mkulima
mkazi wa Kijiji cha Mgama wilaya
ya Iringa amekamatwa na jeshi la polisi mkoani hapa akiwa na
silaha aina ya Shortgun fupi
iliyotengenezwa kienyeji isiyokuwa nan amba za usajili
maarufu kama Kipalupalu akiwa
ameificha ardhini ambayo alikuwa
akiitumiwa kwa matukio ya uhalifu.
Kuwa
mtuhumiwa huyo amedai kuwa amekuwa akiitumia silaha hiyo katika matukio mbali mbali ya uhalifu na alikamatwa
April 5 majira ya saa 6 mchana katika Kijiji hicho na kuwa mtuhumiwa atafikishwa
mahakamani wakati wowote .
Wakati huo
huo jeshi la polisi la
Polisi mkoa wa Iringa limeanza
uchunguzi wa kuhoji taasisi zinazotuhumiwa
kujihusisha na uhamasishaji wa
vitendo vya ushoga na ndoa za jinsia
moja .
0 Comments