Header Ads Widget

NI UKATILI WA KUTISHA IRINGA BABA AMLAWITI MWANAE WA MWAKA MMOJA

 


JESHI la  polisi  mkoa wa  Iringa  linamshikilia  Amani  Martin maarufu kwa  jina la Kasisi (47) mkazi  wa  Nzihi  wilaya ya  Iringa ambae pia ni kiongozi wa dini kwa  tuhuma  za  kumlawiti  mtoto  wake mwenye  umri wa mwaka mmoja  na miezi  saba kwa madai ya  kudanganywa na   shetani.

 

Kamanda  wa  polisi wa  mkoa wa Iringa Allan Bukumbi aliwaeleza  wanahabari leo    ofisini  kwake kuwa   tukio  hilo lilitokea  Machi 28 majira ya saa saba  mchana  na  kumsababishia maumivu makali  sehemu za  haja kubwa .

 

Alisema  kuwa Kasisi ambae ni mkulima  wa  Kijiji  cha Nzihi alidai  kuwa alifanya tukio  hilo baada ya  kudanganywa na  shetani na  kuwa anajutia  kutenda  unyama  huo kwa mwanae .

 

Alisema  kuwa mama wa  mtoto huyo  Magreth Kaguo (29)  ndie  ambae  alibaini  mtoto  wake  huyo  kulawitiwa na  kuwa mtuhumiwa  amekamatwa na atafikishwa mahakamani  wakati  wowote .

 

Katika   tukio  jingine  jeshi la polisi linamshikilia mtuhumiwa mmoja  jina limehifadhiwa   kutokana na sababu za kiuchunguzi ambae  anatuhumiwa  kukodisha silaha  kwa wahalifu .

 

Kamanda Bukumbi  alisema kuwa  mtuhumiwa  huyo mkazi wa eneo la Kihesa Kilimani Manispaa ya  Iringa  alikamatwa  April 3 majira  ya  11  jioni baada ya   taarifa  fichi  kutoka kwa  wasamaria  wema kuhusiana na biashara isiyo rasmi ya  ukodishaji silaha mbili  aina ya  shotgun yenye namba za  usajili TZ CAR 6271 na Rifle yenye namba za usajili CAR 48081 ambayo  imepelekwa kikosi  cha mizinga mkoa wa Morogoro  kwa ajili ya matengenezo ,kuwa  kupitia mwanya  huo amekua akijipatia  fedha  kwa  njia ya  kukodisha silaha  na  risasi  kwa  kiasi cha shilingi 100,000 kwa  tukio .

 

“ mtuhumiwa  huyo  amekuwa akikodisha  silaha  hizo kwa  watu mbali mbali  kitu ambacho  ni kinyume na utaratibu  wa  matumizi ya silaha  na sheria  za  nchi .

 

Kamanda  Bukumbi alisema  tukio  jingine ni lile  lililotokea   April 4 mwaka huu  eneo la Mwangata  A kata ya Mwangata Manispaa ya  Iringa kwa  jeshi  hilo kufanya msako  na kufanikiwa kukamata  silaha  aina ya Pistol Rami yenye namba za usajili A935520 pamoja na risasi  zake 10 ndani ya Magazine  ambayo ilisalimishwa  karibu na nyumba ya mwenyekiti  wa mtaa wa Mwangata  A  Batista Kisonga baada ya mtuhumiwa  Rashid Nyomolelo  kuiba kutoka kwa  Joseph Philipo Lukonde  (44) mkazi wa Nkuhungu mkoani Dodoma mtuhumiwa  bado anatafutwa .

 

Wakati  huo  huo Julius Mlwale(36) mkulima  mkazi wa Kijiji  cha Mgama wilaya ya  Iringa  amekamatwa na jeshi  la polisi mkoani hapa  akiwa na  silaha aina ya  Shortgun fupi iliyotengenezwa  kienyeji  isiyokuwa nan amba  za usajili  maarufu kama Kipalupalu  akiwa ameificha ardhini ambayo  alikuwa akiitumiwa kwa matukio ya uhalifu.

 

Kuwa mtuhumiwa  huyo  amedai kuwa amekuwa  akiitumia silaha  hiyo katika matukio mbali mbali ya uhalifu  na alikamatwa  April 5 majira ya saa 6 mchana katika Kijiji  hicho na kuwa mtuhumiwa atafikishwa mahakamani  wakati  wowote .

 

Wakati  huo  huo jeshi  la  polisi la  Polisi mkoa wa Iringa limeanza  uchunguzi wa  kuhoji taasisi  zinazotuhumiwa  kujihusisha na uhamasishaji  wa vitendo vya  ushoga na ndoa za  jinsia  moja  .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI