Header Ads Widget

RC MGUMBA TANGAZA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA KIPINDI CHA MIAKA MIWILI

NA AMINA SAIDI,MATUKIO DAIMA TANGA

Mkuu wa mkoa wa Tanga Omary Mgumba  ametangaza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita  kwa miaka miwili ambapo alisema wamepokea zaidi sh.bilion 95 kwa ajili ya  uboreshaji wa sekta ya Elimu kutoka kwa Dkt.Samia suluhu Hassan. 

Akizungumza katika Kongamano la kutangaza mafanikio ya serikali ya Awamu sita ndani ya miaka miwili iliyofanyika katika ukimbi wa Legal Naivera   alisema wamefanikiwa kujenga zaidi ya madarasa mapya  16 na madarasa 327 kupitia fedha iliyoletwa na serikali ya awamu ya sita chini ya usimamizi wa Dkt Samia suluhu Hassan. 


Aidha alisema madarasa hayo 16 na madarasa  327 yote yamepokea wanafunzi,lakini pia kupitia fedha hizo wamefanikiwa kujenga mabweni zaidi ya 21na matundu ya vyoo 1774 na nyumba za waalimu 4.


Sambamba na hayo mkuu wa mkoa huyo alieleza kuwa Mapato  katika Halmashauri  zimeongezeka kutoka billion 29 ya mwaka 2021  hadi kufikia billion 35 mwaka 2022.


Aliongeza kusema kuwa sababu za kutangaza mafanikio hayo ni kutokana na taarifa mbalimbali  ya upotoshaji inayovuma mtandaoni ya kwamba serikalj haijafanya jambo lolote hivyo kupitia taarifa hiyo wananchi wamejua kuwa serikali imefanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Tanga  Ustad Rajabu Abdarahman Abdalah alisema kuwa  hayo mafanikio ya serikali  ya awamu ya sita ni utekelezaji  wa ilani ya chama hicho chini mwenyekiti wa CCM  Taifa Dkt.Samia Suluhu Hassan.


Sambamba na hayo aliwakemea wahudumu wa afya ambao wanahatibh trauma yao kwa kutumia  lugha mbaya kwa wagonjwa wakati  wakuwapatia huduma.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS